Sunday 3 August 2014

BUNDUKI ZA STARS KUWAUA MSUMBIJI LEO HIZI HAPA

NGASSA, OSCAR BENCHI, 'VIALLI', MOURAD NDANI..KIKOSI KAMILI KUWACHARANGA MAMBAS


Khamis Mcha "Vialli' (kulia) yupo kamili gado kuwaua Mambas
KOCHA mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mholanzi, Mart Nooij imeamua kumuanzisha mfungaji wa mabao wawili katika mechi iliyopita dhidi ya Msumbiji uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Khamis Mcha ‘Vialli’ badala ya Mrisho Khalfan Ngassa.
Pia Oscar Joshua ataanzia benchi leo hii na nafasi yake itachukuliwa na mpiganaji, Said Mourad Mwenda.
Kikosi kitakachoanza leo dhidi ya Mambas: Deogratius Munish ‘Dida’, Shomar Kapombe, Said Mourad, Kevin Patrick Yondani, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Erasto Edward Nyoni, Thomas Ulimwengu, Mwinyi Kazimoto, John Bocco, Mbwana Samatta na Khamis Mcha ‘Vialli’.
Wachezaji wa akiba wanatarajiwa kuwa: Aishi Manula, Aggrey Morris, Oscar Joshua, Haroun Chanongo, Mrisho Ngassa, Simon Msuva na Amri Kiemba.
Mechi ya kwanza Stars ililazimishwa sare ya mabao 2-2 nyumbani na leo inahitaji kupata ushindi wa aina yoyote ile au sare ya kuanzia mabao 3-3.
Taarifa kutoka msumbiji zinasema kikosi cha Stars kipo salama na wachezaji wote wana morali ya kumcharanga Mambas kuanzia majira ya saa 9:00 alasiri kwa saa za Msumbiji na Tanzania itakuwa saa 10:00 jioni.
Mechi hiyo ya kukata na shoka itapigwa uwanja wa Taifa wa Zimpeto uliopo nje kidogo ya mji wa Maputo

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA