Wednesday 6 August 2014

LAANA YA MAMA YAKE YAMTISHA WEMA SEPETU


NYOTA  wa  Filamu  za  kibongo  Wema  Sepetu  amesema  kuwa  katika  maisha yake  anajitahidi  hakosani  na  mama  yake  mzazi, Mirium Sepetu  ili  kukwepa  kupata  laana  ya  kile  ambacho  anaweza  kumtamkia  na  kuharibu  mwelekeo  mzima  wa  malengo  yake  aliyojipangia  kuyatimiza  akiwa  ndani  ya  ndoa  yake..
.Akizungumza  na  Mpekuzi, Wema  alisema  kuwa  ndio  maana  kipindi  ambacho  mama  yake  hakutaka  kuolewa  na  mchumba  wake  Nasibu  Abdul  'Diamond'  hakupenda  kutumia  nguvu  ama  uwezo  wake  wa  kifedha  kumpuuza  mzazi  wake  kwani  anaamini  angemuumiza  na  kumfanya  amtamkie  maneno  mabaya...



"Natambua  fika  kuwa  Mungu  ametuagiza  kuwaheshimu  wazazi  wetu  kwani  hawa  ni  miungu  wadogo, wakitamka  neno  lolote  baya  baada  ya  kuwaudhi  huwa  linaumbika  na  kuwa  shida  kwa  mhusika, ndio  maana  wakati  anaweka  mikingamo  ya  mimi  kuolewa  na  Diamond  sikulazimisha  bali  niliendelea  kumsihi  akubali." Alisema  Wema.


Penzi  la  Wema  na  Diamond  linazidi  kupamba  moto  hasa  baada ya  hivi  karibuni  kuvishana  pete  nyingine  ya  uchumba  baada  ya  mama  Wema  kubariki  penzi  lao

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA