CHEKI HAPA YALIYOJIRI ENGLAND LEO MANCHESTER UNITED IKIAMBULIA MVUA YA MAGOLI NA MATOKEO MENGINE:
22:27 |
Man United ambao walishinda mechi iliyopita ya ligi dhidi ya QPR kwa ushindi wa magoli 4-0, leo hii wameonja kipigo kizito kutoka kwa Leicester, baada ya kukubali kufungwa 5-3.
Man United ndio waliokuwa wa kwanza kuliona lango la Leicester kupitia Robin van Persie, kabla ya dakika baadae Angel di Maria kuongeza la pili.
Dakika moja baada ya United kufunga goli la pili, Leicester wakafungw goli la
Kwanza kupitia Ulloa na mpaka mapumziko matokeo yalikuwa 2-1.
Kipindi cha pili Ander Hererra akaifungia Man United goli la 3, lakini dakika chache baadae Leicester wakapata penati na kufunga goli la pili, huku United wakiwa bado na hasira za kulalamikia maamuzi ya refa, Estaban Cambiasso akafunga goli la kusawazisha.
Mchezaji aliyeng’ara kwenye mchezo Jamie Vard akaifungia City goli la 4, kabla ya dakika baadae Nugent kufunga goli la tano kwa mkwaju wa penati.
Mpaka refa anapuliza kipenga cha mwisho Leicester City 5-3 Man United.
Katika mechi nyingine goli la Frank Lampard dakika ya 85 liliifanya Manchester City itoshane nguvu na timu ya Chelsea kwa bao moja kwa moja kufuatia goli la Andre schurie uwanja wa Etihad.
Totenham imechapwa bao moja na West Bromich Albion huku Everton ikibugizwa goli 3 kwa mbili na Crystal palace
Related Posts:
CHELSEA YAPIGIKA KWA SWANSEA CITY GOLI 1-0 SWANSEA CITY YAIDUWAZA CHELSEA WAKATI GUUS HIDDINK AKIONJA KIPIGO CHA KWANZA Timu ya Swansea City imepata ushindi wake wa kwanza dhidi ya Chel… Read More
SAMATTA AENDELEZA AKAUNTI YA MABAO GENK IKISHINDA 4-0 MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ametokea benchi na kuifungia timu yake, KRC Genk katika ushindi wa 4-0 dhidi ya KV Oo… Read More
LA LIGA::JINAMIZI LA KIPIGO LAZIDI KUITESA BARCELONA Barcelona imeendelea kutofanya vyema katika Ligi Kuu ya Hispania La Liga baada ya kufungwa na Real Sociedad bao moja bila na kupata mstuko katika mb… Read More
ANDY CAROLL APIGA HAT-TRICK NA KUZIDI KUITIBULIA ARSENAL MAHESABU YA UBINGWA Magoli matatu ya Andy Caroll kwa lugha ya soka hat-trick yameleta pigo kwa timu ya Arsenal ambayo tayari inanafasi finyu ya matumaini ya kutw… Read More
ROBO FAINALI EUROPA::LIVERPOOL YAIBANA DORTMUND UGENINI LIVERPOOL imejiweka kwenye mazingira mazuri ya kwenda Robo Fainali ya UEFA Europa League baada ya kulazimisha sare ya 1-1 ugenini na Bo… Read More