Monday 8 September 2014

MSANII MWINGINE WA BONGO MOVIE AFARIKI DUNIA GHAFLA!


Msanii wa Bongo Muvi, Mariam Juma ‘MC Chimamy’ enzi za uhai wake.

Msiba! Bado bundi wa vifo anaendelea kung’ang’ania tasnia ya sinema za Kibongo kufuatia kifo cha ghafla cha msanii wa Bongo Muvi, Mariam Juma ‘MC Chimamy’ ambaye amefariki dunia ghafla baada ya kupatwa na kifafa cha mimba, ugonjwa uliomkuta muda mfupi kabla ya kujifungua.

Mauti hayo yalimkuta MC Chimamy wikiendi iliyopita baada ya kukimbizwa kwenye Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar, akiwa tayari na hali mbaya kwani kabla ya hapo alianzia Hospitali ya Palestina, Sinza ambapo alilazimika kukimbizwa katika hospitali hiyo ya Wilaya ya Kinondoni ili kunusuru maisha yake na kiumbe alichokuwa nacho tumboni. 

Msiba huo umezua simanzi kubwa kwa wasanii wenzake hasa Vanita Omary, Halima Yahya ‘Davina’, Yvonne-Chery Ngatwika ‘Monalisa’, Mariam Kakwaya na wengine kwani alikuwa ni mtu wao wa karibu na siku aliyokutwa na umauti alikuwa amepangwa kuwa mshereheshaji wa shughuli ya Davina ya kibao kata iliyofanyika Bamaga-Mwenge, Dar. 

“Msiba huu umenishtua sana, sikutarajia kama Chimamy angetutoka kimchezo hivi, ukweli nimeumia sana na sina la kusema, namshukuru Mungu kwa kazi yake,” alisema Vanitha.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA