BREAKING NYUZZZZ..YANGA YAIFANYIA SIMBA UMAFIA...: YAMSAJILII DANNY MRWANDA
10:11 |
No Comments |
Mshambuliaji Danny Mrwanda amemwaga wino wa kuitumikia klabu ya Yanga ya jijini Dar es salaam kwa mkataba wa mwaka mmoja usiku huu.
Yanga imewafanyia umafia watani zao wa jadi Simba,ambayo ilionyesha nia kubwa ya kumuhitaji Mrwanda ikiwa ni kwa hudi na uvumba na tayari ilishatangaza nia yake hiyo ya kutaka kumsajili.
Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Klabu ya Yanga kinasema kuwa,Yanga imeamua kumsajili Mrwanda kuchukua nafasi ya Said Bahanuzi aliyetolewa kwa mkopo kwenda Polisi Morogoro wakati Jerry Tegete akiwa ni majeruhi,na mshambuliaji pekee wa ndani wanayemtegemea ni Hussein Javu.
Yanga imewafanyia umafia watani zao wa jadi Simba,ambayo ilionyesha nia kubwa ya kumuhitaji Mrwanda ikiwa ni kwa hudi na uvumba na tayari ilishatangaza nia yake hiyo ya kutaka kumsajili.
Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Klabu ya Yanga kinasema kuwa,Yanga imeamua kumsajili Mrwanda kuchukua nafasi ya Said Bahanuzi aliyetolewa kwa mkopo kwenda Polisi Morogoro wakati Jerry Tegete akiwa ni majeruhi,na mshambuliaji pekee wa ndani wanayemtegemea ni Hussein Javu.
Mrwanda kutua Yanga SC ni kutimia kwa ndoto zake, kwani wakati anachipukia kisoka aliwahi kwenda kufanya majaribio ya kuomba kusajiliwa, lakini hakufanikiwa mwaka 2005 na karudi AFC ya Arusha.
Mrwanda, mwenye umri wa miaka 31 sasa, aliibukia AFC ya mwaka mwaka 2003 ambako alicheza hadi 2006 alipohamia Simba SC alikocheza hadi 2009 alipokwenda Al Tadamon ya Kuwait.
Alirejea Simba SC mwaka 2009 na akacheza hadi 2010 alipokwenda Vietnam kujiunga na Dong Tam Long An ambayo aliichezea kwa msimu mmoja kabla ya kuhamia Hoang Anh Gia Lai aliyochezea hadi mwaka huu alipojiunga na Polisi Morogoro.
Baada ya kusaini Mkataba huo, usiku huu Mrwanda anakwenda kujiunga na wachezaji wenzake katika hoteli ya Landmark, Mbeazi Beach kwa maandalizi ya mechi ya Nani Mtani Jembe dhidi ya Simba SC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Related Posts:
UEFA::SUAREZ AITETEA BARCELONA ,TORRES AKILIMWA KADI NYEKUNDU MABINGWA wa zamani wa Ulaya, Barcelona ya Hispania na Bayern Munich ya Ujerumani, zote zimepata ushindi mwembamba katika mechi zao za kwanza za R… Read More
UHOLANZI YAILAZA UINGEREZA NYUMBANI KATIKA DIMBA LA WEMBLEY Timu ya Uingereza iliyojaa matumaini baada ya ushindi dhidi ya Ujerumani imejikuta ikifungwa mabao 2-1 katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki dh… Read More
CHAD YAJITOA AFCON 2017 Timu ya Taifa ya Chad ‘Les Sao’ imejiondoa katika michuano ya kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa Afrika (AFCON) itakayofanyika mwaka … Read More
ALIYEKUWA KIPA WA SIMBA, ABBEL DHAIRA AFARIKI DUNIA Dhaira siku za mwisho za uhai wake KIPA wa zamani wa Simba SC, Abbel Dhaira amefariki dunia leo baada ya kusumbuliwa na ugojwa wa saratani ya… Read More
STARS YAVUNJA KAMBI, WACHEZAJI WAREJEA KLABU ZAO Ndoto za mshambuliaji wa Mansfield Town ya Daraja la Pili England, Abdillah Yussuf ‘Adi’ kuichezea Taifa Stars kwa mara ya kwanza zimeyeyu… Read More
0 comments:
Post a Comment