Saturday 27 August 2022

SEHEMU YA KWANZA::NAMNA YA KUONDOA MSONGO WA MAWAZO NA MFADHAIKO


msongo wa mawazo
Mara nyingi sana umesikia mtu akisema “nina stress”, mwingine akasema ana msongo wa mawazo na mara chache katika mazungumzo ukasikia mtu akitumia neno mfadhaiko. Haya ni maneno yanayoingiliana kimazungumzo mitaani na mara nyingi mtu hutumia neno moja katika hayo bila kujua tofauti zake. Katika mada yetu tutayachambua na kujua tofauti za matatizo yanayowasumbua watu hadi kupelekea kuyatumia maneno haya. Na mwisho tutatoa ushauri wa namna ya kuondokana na matatizo hayo.

Kwa Kuanza Tuangalie Maana Ya Stress Au Msongo Wa Mawazo

Maisha ya dunia ya leo yamejaa pilikapilika za kila aina, una vitu vingi vya kuvifanya katika muda uliopangiwa (deadlines), vitu vingi vya kukukatisha tamaa na matakwa mengi ya binafsi na watu walio karibu na wewe. Mtindo huu wa kuishi umekuwa karibu ni wa kila mtu. Kila wakati unakuwa na msongo wa mawazo (Stress). 

Msongo wa mawazo kwa kiasi fulani siyo mbaya, unakusaidia kutekeleza majukumu yako ukiwa umebanwa na kukupa nguvu ya ziada ya kuyafanya vizuri kadiri ya uwezo wako. Lakini kama utaendelea kufanya shughuli zako kwa mtindo huu, wakati utafika ambapo ubongo wako utachoka na kupata tatizo la kiafya linaloitwamfadhaiko (Depression).

Kwa hiyo msongo wa mawazo (Stress) ni namna ya kawaida ya mwili wako kukabiliana na mambo ya kukutisha au kukufanya uwaze.
Unapohisi hatari, ya kweli au siyo ya kweli, mwili hukupa nguvu haraka kukabilina na suala lililopo mbele yako, hii ni ni namna ya mwili wako kukulinda. Katika mazingira hayo, mwili hukufanya uwe mwangalifu zaidi na kukupa nguvu ya ghafla. 
Katika mazingira ya hatari, unaweza kuokoa maisha yako kwa kupata hiyo nguvu na ujasiri wa ghafla. Mfano mzuri ni pale unapoendesha gari na ghafla ukakanyaga breki za gari kuzuia ajali mbele yako.
Msongo wa mawazo hukusaidia kukabiliana na vikwazo mbalimbali. Utakuwa makini sana wakati unawasilisha mada mbele ya kadamnasi, utakuwa na umakini zaidi wakati unashiriki kwenye mechi na timu pinzani na utasukumwa kwenda kusoma ili ujiandae kwa mitihani yako badala ya kuangalia kipindi kizuri cha kwenye luninga unachokipenda.
Lakini kama tulivyodokeza hapo awali, kiwango cha msongo wa mawazo kikizidi, badala ya kukusaidia kitakuletea matatizo ya afya, kitaathiri utendaji wako wa kazi, kitavuruga mahusiano yako na wengine na kudunisha maendeleo yako ya maisha.
USIKOSE SEHEMU YA PILI
credit: topantiagingproducts

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA