Friday 5 December 2014

MSHTUKO! ISLAMIC STATE (IS) WAFUNGUA KAMBI YA MAFUNZO AFRIKA...NI LIBYA!



Wapiganaji wa Islamic State katika jimbo la Anbar,Syria Marchi 2014
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wafungua kambi za mafunzo LibyaWapiganaji wa kundi la Islamic State wameanzisha kambi za mafunzo mashariki mwa Libya, amesema mkuu wa kamandi ya Marekani ya masuala ya Afrika. 
Wapiganaji wa Kikurd wakiwa katika mafunzo ya kijeshi kukabiliana na wapiganaji wa Islamic State Septemba 2014 nchini Iraq.Jenerali David Rodriguez amesema kuna mamia ya wapiganaji wa IS wanaopata mafunzo ya kijeshi kwenye kambi zake nchini Libya. Amesema kambi hizo zipo katika hatua za mwanzo kabisa, lakini Marekani imekuwa ikiyafuatilia kwa karibu kuona zinavyoendelezwa.
Libya imekuwa katika mgogoro tangu kuangushwa kwa utawala wa Muammar Gaddafi mwaka 2011, ambapo makabila mbalimbali, wanamgambo na makundi ya kisiasa, wote wakipigania madaraka.
Makundi mbalimbali ya Kiislam yanawania madaraka mashariki mwa Libya, hukubaadhi yakitangaza kuwa na ushirikiano la kundi la Islamic State, IS. 
Wapiganaji kutoka kikundi cha IS wakipakia mabaki ya kile kinachosemekana kuwa mabaki ya ndege ya Marekani isiyotumia abiria baada ya kukonga katika mnara wa mawasiliano huko Raqqa Septemba 23,2014Akizungumza mjini Washington Jumatano, Jenerali Rodriguez bado haijafahamika ukaribu uliopo kati ya watu wanaopata mafunzo hayo na kundi la IS."Kikubwa ni watu wanaokuja kupata mafunzo na msaada wa vifaa kwa ajili ya kambi za mafunzo kwa sasa," amesema. "kwa sasa mafunzo hayo bado ni ya hatua ya chini sana na tunafuatilia kuona namna hali inavyokwenda." 
-MATUKIOTZ

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA