Thursday 19 March 2015

MAREKANI YAFUNGUKA "TUMEMUUA KIONGOZI WA ALSHABAAB

Image result for al shabaab
Wizara ya ulinzi nchini Marekani imethibitisha kwamba imemuua mojawapo ya viongozi wa kundi la wapiganaji wa Somalia Al Shabaab kupitia kombora.
Adan Garaar alituhumiwa kupanga shambulio katika jumba la kibiashara la West Gate nchini Kenya miaka miwili iliyopita.
Maafisa nchini Marekani wanasema aliuawa kusini mwa Somalia ijumaa iliyopita.
Marekani imekuwa ikikagua operesheni hiyo kabla ya kuthibitisha kwamba Garaar ndiye aliyekuwa akilengwa.
Nchi hiyo imewalenga viongozi wengine wakuu katika kundi hilo la wapiganaji wenye itikadi kali za kiislamu kwa mkombora akiwemo kiongozi wa zamani wa kundi hilo, Ahmed Godane.
-BBC

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA