Tuesday 4 August 2015

LOWASSA RASMI MGOMBEA URAIS KUPITIA CHADEMA

  Mkutano Mkuu wa CHADEMA umempitisha Edward Lowassa kuwa Mgombea Urais na mgombea mwenza Duni Haji, hatimaye kuwa wagombea wa UKAWA.
CHADEMA imewapokea rasmi na kuwakabidhi kadi viongozi kadhaa mashuhuri waliokuwa CCM na ambao wamejiunga na CHADEMA.Wamekabidhi kadi viongozi wanne wanaowakilisha makundi kadhaa yaliyojiorodhesha kujiunga CHADEMA.Kadi ya kwanza imetolewa kwa Mgana Msindai Mwenyekiti wa Wenyeviti wa mikoa wa CCM akiwakilisha wenyeviti kadhaa walioomba kujiunga CHADEMA.Kadi ya pili amekabidhiwa Makongoro Mahanga Naibu Waziri wa Kazi na Ajira kwa niaba ya mawaziri na manaibu waziri kadhaa walioomba kujiunga na jeshi la ukombozi.Kadi ya tatu imetolewa kwa Mbunge wa Arumeru Magharibi Ole Madeye akiwakilisha wabunge wengi walioomba kujiunga CHADEMA.Kadi ya nne imetolewa kwa Katibu wa fedha na Uchumi CCM Kahama ambaye anawakilisha viongozi wa wilaya kwa mamia ambao mpaka sasa wameorodhesha majina yao ili wasimame wahesabiwe!
      

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA