Sunday 1 November 2015

LIVERPOOL YAITWANGA CHELSEA 3-1, SASA MOURINHO ASOGEA MLANGO WA KUTOKEA

Liverpool boss Jurgen Klopp celebrates winning at Chelsea
Kocha wa Liverpool akipongezana na beki Sakho 
Philippe Coutinho scores his second goal for Liverpool at Chelsea
Coutinho akipiga shuti kupachika bao la pili mbele ya nahodha Terry

Chelsea ikiwa nyumbani  nyumbani imelala kwa mabao 3-1.


Liverpool ndiyo waliowatandika Chelsea kwa mabao hayo hali ambayo inamuweka Kocha Jose Mourinho katika hali ya sintofahamu na kusogea zaidi mlango wa kutokea.



Chelsea ilianza vizuri  wakati Ramires akipachika bao la  kuongoza baada ya dakika tatu tu bali imani ya  Liverpool haikupotea na a Philippe Coutinho aliisawazishia kwa mkwaju maridadi  katika kipindi cha kwanza mwishoni.

Baada ya mapumziko Coutinho tena aliiweka Liverpool mbele kwashuti kali lililombabatiza  John Terry na dakika 16 baadae Christian Benteke alipachika bao la tatu na mpira kumalizika kwa  ushindi wa kocha  Klopp ushindi ambao alistahili.

Ramires akishangalia baada ya kuipatia Chelsea bao la kuongoza

Ushindi wa Liverpool unaongeza shinikizo kwa meneja wa Chelsea Jose Mourinho ambaye klabu yake imeshindwa kabisa kutamba msimu huu.
Matokeo kamili ya mechi za Jumamosi ni kama ifuatavyo:
Chelsea 1-3 Liverpool
Crystal Palace 0-0 Man Utd
Man City 2-1 Norwich
Newcastle 0-0 Stoke
Swansea 0-3 Arsenal
Watford 2-0 West Ham
West Brom 2-3 Leicester




0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA