Wednesday 2 December 2015

RAIS WA CHINA AZURU ZIMBABWE

Xi Jinping akitumbuizwa nchini Zimbabwe
Rais wa China Xi Jinping yuko nchini Zimbabwe katika ziara ya siku mbili inayolenga kujenga mahusiano na Zimbabwe.
Rais huyo anatarajiwa kufanya mkutano wa moja kwa moja na mwenyeji wake hii leo rais Robert Mugabe.
Jinping ndiye rais wa kwanza wa China kufanya ziara nchini Zimbabwe katika kipindi cha takriban miaka 20
Xi akikagua gwaride la heshima Zimbabwe
Rais huyo wa China amepokelewa kwa shangwe na taadhima katika uwanja wa ndege wa kimataifa na raia waliojawa na furaha wakiongozwa na rais Mugabe.
Maafisa nchini Zimbabwe wanatarajia kuwa makubaliano kadha yenye thamani ya mabilioni ya pesa yatatiwa sahihi yakiwemo mikataba ya ujenzi wa miundo msingi, kilimo na vilevile katika sekta ya uchukuzi.
Maafisa nchini Zimbabwe wanatarajia kuwa makubaliano kadha yenye thamani ya mabilioni ya pesa
Lakini wanasiasa wa upinzani wamepuuzilia mbali ziara hiyo wakisema kuwa Uchina, haitawekeza hadi chama tawala cha ZANU-PF kiamue ni nani mrithi wa Mugabe ambaye sasa ana umri wa miaka tisini na moja.
Uwekezaji wa China barani Afrika ulidorora kwa zaidi ya asilimia 40 miezi sita ya kwanza ya mwaka huu kutokana ukuaji mdogo wa uchumi nchini humo.
-BBC

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA