Friday 11 March 2022

WEEKEND VIBES::::ACHA HARAKA, JIFUNZE KUSUBIRI


 Ni jambo la kumshukuru Mungu kwamba tumekuwa miongoni mwa waliochaguliwa kuuona mwezi huu, ingawa yatupasa tuombe sana ili mwaka huu uwe wa baraka kwetu. Maana mnajua kwa kiasi gani wapendwa wetu walivyopotea na hatutawaona tena.
 
Leo nikwa ofisini nilikuwa natafakari stori kadhaa za washkaji wanaolaumu kupigwa mizinga na "mademu" zao, halafu nikwaza wakati fulani kuna mabinti wakati tukipiga stori walisema kuwa wanaume tuna haraka sana ya tendo hata kabla uhusiano haujakomaa, haha nakumbuka yule mdada alisema "Mhmhm jamani mtu hata wiki haijaisha kisa nimemkubali ndio anataka tuanze kuminyana ,aisee mimi sipendi kabisa"........ Hapa jibu moja tu limepita kichwani, SUBIRA...
Mada yangu leo kama unavyoweza kuiona hapo juu kwenye kichwa  cha habari, inawazungumzia zaidi akina dada, kwa sababu zilizo wazi kabisa kwamba, wao ndiyo maua ya dunia, bila wenyewe hata maisha sijui yangekuwaje ,lakini sijasahau kaka zangu kwani sote tunategemeana.
Ni jambo la kweli kwamba mara nyingi wanaume ndiyo wanaokuwa wa kwanza kutangaza nia kwa mwanamke tofauti na inavyokuwa kinyume chake. Inapotokea mwanamke ‘anamtokea’ mwanaume, huwa ni gumzo na siyo ajabu kukuta mwanaume akikataa, anaona kama vile anategewa au mwanamke anayemtongoza ana kasoro.
Kwa wanaume, wengi wao hupenda baada ya kukubaliwa katika kutongoza kwao, kinachofuata kiwe ni tendo la ndoa na si vinginevyo wakati kwa wanawake, baada ya kukubaliwa, wao hupenda kwanza wazoeane kwa maongezi, vijizawadi na mitoko ya hapa na pale kabla ya kuhitimisha kwa tendo. Hii ni hulka ambayo imeendelea hadi kujenga mazoea, kiasi kwamba wanaume wakimpata mwanamke wa kushiriki naye tendo siku ya kwanza tu ya kukutana kwao, huwaona kama wasiofaa. Wamezoea wakikubaliwa, wazungushwe japo siku mbili tatu kabla ya kumalizana.
Sasa utamu unakuja pale mwanaume baada ya kukubaliwa, kwa kawaida, atatoa mwaliko kwa mwenzake kwa ajili ya mazungumzo, mara nyingi huwa ni hotelini kwa ajili ya chakula cha mchana au kwa wanywaji basi hukutana eneo zuri kwa ajili ya kujipatia mbili tatu.
Inaweza kuwa siku ya kwanza, ya pili na pengine kwa siku kadhaa. Katika kipindi hicho, mwanaume atakuwa ametoa ofa kama hivyo ya vinywaji, vocha na hata pesa kwa mwenza wake. Uzoefu unaonyesha kuwa mara nyingi wakaka wanapoulizia kuhusu faragha, hukutana na maswali au majibu kama “yaani mbona wewe una haraka? Harakaharaka haina Baraka”.
Na hata wengine huwaambia maneno kama “Yaani wewe hicho ndicho unachokiwaza.” Kauli hizi za akina dada huwa na nia ya kupunguza spidi ya jamaa wenye uchu. Kama nilivyodokeza pale juu, kwa mujibu wa mazoea yaliyojengeka, inatarajiwa kuwa walio katika uhusiano watachukua muda kidogo kabla ya kufikia hatua ya kushiriki tendo.
Lakini wakati akina dada wamekuwa wakisisitiza kutokuwa na haraka ya kushiriki tendo kwenye uhusiano mpya, uzoefu pia unaonyesha wao huwa hawasubiri kabla ya kuanza mambo yao. Katika siku ya kwanza ya kutongozwa na kukubali, kesho yake wataanza kuomba vocha. “Baby naomba vocha niongee na mama, yaani nimemmiss sana,” utasikia msichana akimwambia mpenzi wake. Baadhi hununua muda wa maongezi kweli, lakini wengi wao hutuma hela kutegemea na uzuri wa mdada.
“Baby naomba niongezee elfu ishirini kuna kitu nataka kununua hapa nitakurudishia..” wengine huja na kauli kama hizi. Kifupi ni kwamba wasichana wengi huwasumbua wenza wao wapya kwa staili kama hii. Maombi kama haya huwafanya wanaume wahangaike sana kuwatimizia wapenzi wao, lakini pia huwaumiza sana kisaikolojia.
“Hivi kama huyu anaanza kupiga mizinga hata hatujafahamiana vizuri, hivi akishakuwa mpenzi wangu si ndo balaa,” baadhi ya akina kaka hujiuliza.
  Inafika mahali kama huna cha kutoa basi inabidi usugue benchi mpaka upate,,Duh !! Hii hatari sana.
Ngoja nirejee kauli yangu tena,SUBIRA. Sote tusipokuwa wavumilivu kidogo na kujenga uwezo wa kuzishinda tamaa zetu za kimwili na kifedha hakika mambo yataenda sawa .
Sikatai kwamba zawadi zisitolewe au watu msiwe na faragha lakini kila jambo linawakati wake,kama huyo mpenzi siyo wa mpito basi kila hatua ipigwe kwa wakati sahihi Ukiona ana haraka sana SHTUKHAAAA!!!!!!.

Ifike mahali Pesa na zawadi visiwe mtihani kwa mwanaume ili avune pendo na vile vile ngono isiwe mtihani kwa mwanamke ili apate pesa na zawadi.  

Kwa maoni  na ushauri tuwasiliane - Dickson Mulashani -(KD MULA)

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA