Saturday 2 January 2016

MAMLAKA YA MAJISAFI NA USAFI WA MAZINGIRA IFAKARA (IFUWASA) YAUNDA MPANGO WA MAENDELEO KWA MWAKA 2014 HADI 2017



Picha toka maktaba
    
Na Tadeo Jackson,Ifakara                       
Mamlaka ya majisafi  na usafi wa mazingira  Ifakara (IFAUWASA) Imeunda mpango wa maendeleo kwa mwaka 2014 hadi 2017 ambao utaongeza usambazaji  wa maji    katika halmashauri ya mji wa Ifakara wilayani Kilombero.

 Bwana Akley Galawika  ambaye ni meneja amesema kuwa malengo makuu ya mpango huo ni kuongeza maji yanayozalishwa kwa kutumia pampu za umeme ili kuweza kusukuma maji kutoka kwenye visima na kurahisisha upatikanaji wa maji kwa matumizi ya kawaida,pia kuboresha uondoaji wa  maji taka katika halimashauri ya mji wa  ifakara kwa kutumia  gari. 

Vilevile malengo mengine ya mradi  huo  ni kuboresha mtandao wa usambazaji wa maji kwa kutumia mpango wa Kiburubutu na kuhakikisha kuwa wananchi wanapata maji safi na salama ili kupunguza  tatizo la uhaba wa maji.
Aidha Bwana Galawika  amesema katika halmashauri ya mji wa Ifakara kuna jumla ya visima 185 ambavyo viko chini ya serikali, kati ya hivyo 52 ni vibovu kabisa na vinatakiwa kufanyiwa matengenezo,na kuboresha visima vingine.
 Mpango wa maendeleo ambao  uko chini ya mamlaka ya (IFAUWASA) utaanzia Mhola na Lipangalala na utagharamu kiasi cha bilioni sita pointi saba.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA