Friday 12 February 2016

WAZIRI MKUU AAGIZA MIANYA YA WIZI WA MAFUTA IDHIBITIWE

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Mhandisi, Aloys Mtei (kulia) kuhusu  mabomba yanayotawanya mafuta kwenda kwenye matangi makubwa ya makampuni mbalimbali kwenye eneo la Kigambo jijini Dar es salaam Februari 11, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Mhandisi, Aloys Mtei (kulia) kuhusu mabomba yanayotawanya mafuta kwenda kwenye matangi makubwa ya makampuni mbalimbali kwenye eneo la Kigambo jijini Dar es salaam Februari 11, 2016
WAZIRI Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ameitaka Mamlaka ya Bandari nchini (TPA) na Wakala wa Vipimo (WMA) kuhakikisha mafuta yanayoingia nchini yanasafirishwa na kupimwa kwa usahihi ili kuiwezesha Serikali kupata kodi sahihi.
Akizungumza wakati wa kukagua mifumo ya upokeaji, usafirishaji na upimaji wa mafuta yanaposhushwa melini Mhe. Majaliwa amesisitiza umuhimu wa taasisi za serikali zinazosimamia suala hilo kufanya kazi kwa umoja ili kuokoa mapato yanayoweza kupotea kwa sababu za wizi.
IMGS3813
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua eneo lenye mabomba yanayotumika kupitisha mafuta kutoka kwenye meli  kupitia bandari ya Dar es slaam wakati alipofanya ziara ya kukagua miundombinu yenye mianya ya ukwepaji kodi hasa kwenye mafuta yanayoingia nchini Februari 11, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Aidha ameagiza mabomba ya kusafirisha mafuta kwenda kwenye matanki yaliyojengwa katika eneo la Kigamboni yasiosimamiwa na TPA yabomolewe katika kipindi cha mwezi mmoja.
“Nakuagiza  Msajili wa Hazina vunja mkataba wa ubia kati ya Serikali na kampuni ya ORYX zinazomiliki (TIPPER) ili Serikali iwe na kampuni yake yenyewe itakayopokea na kuhifadhi mafuta badala ya iliyopo sasa ya TIPPER inayoendeshwa kwa ubia.
Ameagiza kuanzia sasa utaratibu wote wa kusafirisha mafuta kutoka katika meli kwenda kwenye matanki kwa wafanyabiashara wote usimamiwe na TPA.
IMGS3773
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua flow Meter ya Mafuta ya kupikia ambayo matumizi yake yalizuiwa na Wakala wa Vipimo na Mizani kwa madai kuwa ilikuwa na kasoro. Wapili kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo na Mizani, Magdalen Chuwa.
Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amemhakikishia Waziri Mkuu Majaliwa kuwa TPA imejipanga vizuri kuhakikisha mafuta yanayoingia nchini yanasafirishwa na kupimwa kwa usahihi ili Serikali ipate kodi stahili na imejenga mtambo mpya eneo la Kigamboni utakaosafirisha na kupima mafuta yote utakaoanza kazi mwezi Machi, 2016.
Katika hatua nyingine Waziri Prof. Mbarawa ametembelea Chuo cha Mabaharia  cha Dar es salaam (DMI), na kusisitiza umuhimu wa chuo hicho kuongeza fursa za wanafunzi na walimu  ili kuvutia watu wengi kusoma masomo ya ubaharia na huduma za meli.
Prof. Mbarawa amemwagiza Kaimu Mkuu wa Chuo hicho Eng. Yassin Songoro kutafuta wabia wazuri watakaowezesha chuo hicho kujenga majengo ya kisasa yanayoendana na mitambo ya kisasa iliyopo ya kufundishia.
IMGS3755
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitaka maelezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo na Mizani, Bibi Magdalena Chuwa (kulia) kuhusu sababu zilizomfanya azuie matumizi ya flow Meter katika kuhakiki kiwango cha mafuta yanayoingia nchini kupitia bandari ya Dar es salaam wakati alipofanya ziara kwenye bandari hiyo Februari 11, 2016.
“Mnayo mitambo mizuri ya kufundishia hivyo ongezeni fursa za wanafunzi na walimu ili sekta ya huduma za meli na ubaharia nchini ipate wataalam wengi na kukuza uchumi wa chuo chenu na taifa”, amesema Prof. Mbarawa.
Aidha amekitaka chuo hicho kuwa na uhusiano mwema na vyuo vya aina hiyo duniani ili kubadilishana uzoefu katika mafunzo na kunufaika kimiundombinu na kitaaluma.
IMGS3745
Waziri Mbarawa amesisitiza umuhimu wa kutangaza kozi zinazotolewa chuoni hapo na faida zake ili kuwavutia vijana wengi kusoma taaluma za meli na bahari.
Chuo cha Mabaharia DMI kilichiopo Dar es Salaam kilianzishwa mwaka 1991 kwa sheria namba 22 ya Bunge na kinatoa kozi za msingi kuhusu usafiri wa majini na uhandisi wa meli katika ngazi za cheti, stashahada na shahada.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
IMGS3729
Wazri Mkuu,Kassim Majaliwa na Waziri wa Ujezi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa (kulia) wakimsikiliza Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Mhandisi, Aloys Mtei wakati alipotoa maelezo kuhusu uingizaji wa mafuta kutoka nje ya nchi kupitia bandari ya Dar es salaam Februari 11, 2016.Mheshimiwa Majliwa alikuwa katika ziara ya kukagua miundombinu yenye mianya ya ukwepaji kodi kwenye mafuta yanayoingia nchini kupitia bandari hiyo. 
IMGS3859
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akionyeshwa na kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya bandari Tanzania, Mhandisi Aloys Mtei eneo zinakotia nanga meli kubwa zinazoleta mafuta nchini kupitia bandari ya Dar es salaam Februari 11, 2016.
IMGS3872
WaziriMkuu, Kassim Majaliwa akikagua ujenzi wa Flow Meter eneo la Kigamboni jijini Dar es salaam Februari 11, 2016. Mtambo huo utatumika kupima wingi wa mafuta yanayotoka kwenye meli na kuingizwa hapa nchini. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Raymound Mushi.
 (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA