Tuesday 2 February 2016

WHO YAHOFU VIRUSI VYA ZIKA KUSAMBAA KWA KASI


kipaumbele kimetolewa kulinda Wanawake wajawazito dhidi ya virusi vya Zika
Wataalam wa maswala ya afya wa shirika la Afya duniani WHO wanahofu kuwa virusi vinasambaa mbali na kwa haraka,vikisababisha madhara makubwa.
maambukizi yamekuwa yakihusishwa na maelfu ya watoto wanaozaliwa wakiwa na vichwa vidogo.
tahadhari ya WHO kuhusu Zika ni ya hali ya juu sawa na ya Ebola hii inamaanisha kuwa utafiti na msaada itatolewa kwa haraka kupambana na maambukizi.
Mkurugenzi mkuu wa WHO, Margaret Chan amesema nguvu ya pamoja inahitajika kupambana na virusi hivyo amesema masuala yanayopewa kipaumbele ni kuwalinda wanawake wajawazito na Watoto dhidi ya mbu wanaosambaza virusi.
Tangu mwezi Oktoba kumekuwa na ripoti ya kesi 4,000 za watoto kuzaliwa wakiwa na vichwa vidogo nchini Brazil pekee. 
-BBC

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA