SIMBA YAITUMIA MBEYA CITY KAMA NGAZI KUPANDA KILELENI MWA LIGI
Awadh Juma na Daniel Lyanga kulia wakishangilia na Ibrahim Hajib aliyepiga magoti baada ya kufunga bao la pili dakika ya 90. Kushoto ni kipa wa Mbeya City, Hannington Kalyesebula akiwa amepiga magoti |
SIMBA
SC imefanikiwa kurejea kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara
kufuatia ushindi wa 2-0 dhidi ya Mbeya City Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.
Shukrani
kwao, washambuliaji Ibrahim Hajib na Daniel Lyanga aliyetokea benchi
kipindi cha pili na waliofunga mabao hayo, yanayoifanya Simba sasa
ifikishe pointi 48, baada ya kucheza mechi 21.
Mabingwa watetezi, Yanga na Azam FC wenye pointi 47 za mechi 20 kila mmoja, wanafuatia katika nafasi ya pili nay a tatu.
Lyanga
aliyempokea winga Mganda, Brian Majwega mwanzoni mwa kipindi cha pili,
alifunga bao la kwanza dakika ya 75 akimalizia mpira uliotemwa na kipa
Mganda, Hannington Kalyesebula baada ya Awadh Juma kuunganisha krosi ya
Ibrahim Hajib.
Hajib akafunga la pili dakika ya 90 baada ya kuwatoka mabeki wa Mbeya City na kupiga shuti la mbali kama krosi, lililotinga nyavuni moja kwa moja.
Hajib akafunga la pili dakika ya 90 baada ya kuwatoka mabeki wa Mbeya City na kupiga shuti la mbali kama krosi, lililotinga nyavuni moja kwa moja.
Simba ingeweza kushinda mabao zaidi kwenye mchezo huo kama ingetumia vizuri nafasi ilizotengeneza tangu kipindi cha kwanza.
Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Vincent Angban, Emery Nimubona/Hassan Kessy dk68, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Novaty Lufunga, Juuko Murshid, Justice Majabvi, Mwinyi Kazimoto, Jonas Mkude, Hamisi Kiiza/Awadh Juma dk59, Ibrahim Hajib na Brian Majwega/Daniel Lyanga dk46.
Mbeya City: Hannington Kalyesebula, Hassan Mwasapili, Abubakar Shaaban, Tumba Swedi, Haruna Shamte, Kenny Ally, Raphael Alpha, Haruna Moshi/Themi Felix dk68, Geofrey Mlawa, Joseph Mahundi na Ditrim Nchimbi/Ramachani Chombo ‘Redondo’ dk83.
0 comments:
Post a Comment