HIVI NDIVYO MCHEZAJI PATRICK EKENG RAIA WA CAMEROON ALIVYOFARIKI BAADA YA KUANGUKA DIMBANI
Mchezaji wa Dinamo Bucharest, Patrick Ekeng, amefariki dunia baada ya kupatwa na shambulio la moyo na kuanguka uwanjani.
Ekeng ambaye pia ni kiungo wa timu ya taifa ya Cameroon alianguka uwanjani dakika ya 70 ya mchezo wa ligi ya Romania baina ya Dinamo na Viitorul.
Saa mbili baadaye ilielezwa kuwa Ekeng amefariki dunia hospitalini baada ya kukimbizwa kwa matibabu zaidi.
Shirikisho la Soko la Romania, limetangaza kusitisha michezo yote ya ligi ya nchi hiyo ya mwishoni mwa wiki hii.
Patrick Ekeng akiwa amelala chini baada ya kuanguka dimbani
Patrick Ekeng akiwa amelala chini baada ya kuanguka dimbani
CHINI NI VIDEO YA TUKIO HILO LA KUSIKITISHA
0 comments:
Post a Comment