Wednesday 18 May 2016

WATUHUMIWA WA UBAKAJI, UDHALILISHAJI WAPANDISHWA KIZIMBANI MOROGORO

Watuhumiwa  Zuberi Thabit mkazi wa Mbalizi mkoani Mbeya na Idd Adamu, mkazi wa Iringa, leo wamepandishwa kizimbani kwa tuhuma za kumbaka na kumdhalilisha mwanamke mmoja (jina linahifadhiwa) wa Dakawa mkoani Morogoro, tukio linalodaiwa kufanywa wiki mbili zilizopita katika nyumba moja ya kulala wageni.

Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Morogoro, maofisa wa mahakama hiyo waliwaambia waandishi wa habari kuwa kesi hiyo itasikilizwa faragha ili kutoa nafasi kwa watu wote kutamka maneno na kuona vielelezo bila hofu, hivyo hawataruhusiwa kusikiliza.

Kesi hiyo inayosikilizwa na hakimu Mary Moyo imevuta hisia za wakazi wengi wa mjini hapa, hasa baada ya tukio hilo kusambaa kwa kasi kubwa katika mitandao ya kijamii na simu za mikononi.

Awali, ilidaiwa kuwa Zuberi Thabit ambaye ndiye mtuhumiwa wa ubakaji, ni dereva wa trekta aliyeenda huko Dakawa kwa ajili ya kazi za kilimo, sawa na Idd Adam na akiwa huko, ndiko alimpata mwanamke huyo na kumfanya kuwa mpenzi wake.

Baada ya kumaliza mkataba, inadaiwa Thabit alimtaka mpenzi wake huyo kwenda nyumba moja ya kulala wageni kwa lengo la kuagana, lakini wakiwa wanafanya mapenzi, ghafla alijitokeza Idd ambaye alikuwa uvunguni, aliyeibuka na kuanza kuwarekodi huku wakimtisha kwa kisu binti huyo

Inadaiwa kwamba baada ya kumaliza ‘recording’ hiyo, wanaume hao walitimka zao, lakini wiki mbili baadaye, wakawatumia video marafiki zao wa Dakawa, wakiwa na lengo la kuwadhihaki kwa kumdhalilisha dada yao.
Safari ya kuelekea kizimbani ikiwa imeiva.

Zuberi Thabit mtuhumiwa wa ubakaji.
Idd Adamu mtuhumiwa wa kurekodi video za ubakaji.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA