YAJUE HAYA KUHUSU VAN GAAL NA REKODI YAKE KUHUSU MANCHESTER UNITED
Louis Van Gaal ameiongoza timu hiyo katika michezo 103 na kuiwezesha kushinda 54 , kutoa suluhu 25 na kupoteza 24.
Louis Van Gaal ameiwezesha manchester united kutwaa taji la 12 la
FA na taji pekee katika michuano hiyo tangu Sir Alex Fergurson alipofanya hivyo mwaka 2004.
Van Gaal ameiwezesha timu hiyo kutwaa kombe la fa tarehe 21
/05 /2016 na kufukuzwa kazi tarehe 23 / 05 /2016 akwa ameingia kwenye rekodi ya
kocha kutimuliwa kazi ndani ya siku mbili tangu awezeshe timu yake kutwaa
kikombe.
VanGaal amepewa £ 5million kama sehemu ya kuvunja mkataba pamoja na £ 400,000 ikiwa ni pesa zinazoambatana na zawadi za ushindi wa kombe la FA.
Manchester united imekuwa
klabu ya pili ambapo Van Gaal amepata mafanikio kiduchu kulinganisha vilabu vyote
vitano alivyofundisha na kujizolea vikombe 20 huku kimoja pekee kikiwa kutoka
Old Trafford.(Ajax-11), (Barcelona-4), (AZ Alkmaar-1), (Bayern
Munich-3).
0 comments:
Post a Comment