MAELFU WAMSWALIA MUHAMMAD ALI MWILI KUZIKWA IJUMAA HII
Jeneza lillobeba mwili wa Muhammad Ali |
Maombi
ya Kiislamu ya kuswaliwa kwa jeneza lilobeba mwili wa bondia mashuhuri duniani
marehemu Mohammed Ali yamefanyika katika jimbo la Kentucky, Marekani. Ali
alifariki wiki iliyopita akiwa na umri wa miaka 74.
Maelfu
ya watu, wakiwemo Waislamu kutoka maeneo mengi duniani, wamehudhuria swala hiyo
katika ukumbi wa Freedom Hall, mjini Louisville. Swala hiyo ilirushwa moja kwa
moja kupitia runinga na Waislamu wengi duniani wanatumai kwamba hatua hiyo
inaashiria mchango mzuri kwa dini ya Kiislamu nchini Marekani. Muhammad Ali
alisilimu akiwa kijana.
Alikuwa
kwanza mwanachama wa madhehebu ya Nation of Islam, kundi lililotetea haki za
watu weusi, lakini baadaye akakumbatia imani ya kawaida ya
Kiislamu. Mazishi yake yatafanyika Ijumaa hii.
Baadhi
ya waumini wa Kiislam walioshiriki ibada ya kuuswalia mwili wa Muhammad
Ali
Jeneza lililobeba mwili wa Muhammed Ali likiingizwa msikitini tayari kwa kisomo maalum
Kaka wa Muhammed Ali, Rhaman Ali akielekea msikitini kuwahi kisomo cha mdogo wake
Jeneza lililobeba mwili wa Muhammed Ali likiingizwa msikitini tayari kwa kisomo maalum
Kaka wa Muhammed Ali, Rhaman Ali akielekea msikitini kuwahi kisomo cha mdogo wake
Mke wa pili wa zamani wa Ali, Khalilah Camacho-Ali (kushoto), akisimama karibu na mke mwenza Lonnie Ali ambaye ni mke wa nne
Veronica Porche-Ali (kushoto), mke wa zamani wa Muhammed Ali
Binti wa Muhammed Ali, Laila Ali akiwa amembeba mtoto wake wa kike
0 comments:
Post a Comment