WAFANYAKAZI TBL WASHIRIKI KUISHANGILIA TAIFA STARS
Kundi la washabiki wakishangilia kwa mbwembwe wakati wa mchezo huo
|
Licha ya Taifa Stars kupoteza mchezo wake
dhidi ya timu ya Taifa ya Misri watanzania wengi walikuwa wamejitoa kwa kila
hali kuishangilia katika mchezo huu wa nyumbani uliokuwa unafuatiliwa kwa
karibu na wapenzi wa soka nchini kote.
Katika kuhakikisha wachezaji wa Taifa Stars
wanaongezewa hamasa ya kucheza kwa kushangiliwa, kampuni ya TBL Group ambayo ni
mmoja wa wadhamini wa timu ya taifa mwishoni mwa wiki iliwawezesha baadhi
ya wafanyakazi wake ,familia zao na baadhi ya mawakala wa kuuza bidhaa zake
kuangalia mpambano wa Taifa Stars na timu ya taifa ya Misri.
Lengo kubwa la kuwapatia tiketi za mchezo
wafanyakazi wake na baadhi ya wateja lilikuwa ni kuiongezea nguvu Taifa Stars
kwa kuishangilia.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa na
msisimko mkubwa na kuwavutia maelfu ya washabiki wa soka nchini Taifa Stars
ilifungwa mabao 2-0 na timu ya Misri ‘The Pharaohs’
0 comments:
Post a Comment