Saturday 18 June 2016

WANACHAMA WA CHAMA CHA WAAJIRI WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO TBL

Meneja usalama ,afya na mazingira wa TBL Group Renatus Nyanda,akitoa mafunzo kwa wanachama wa Chama cha waajiri Tanzania( ATE) wakati walipokwenda kujifunza mambo mbalimbali yanayohusiana na usalama sehemu za kazi kwenye kiwanda cha  TBL Ilala jijini Dar es Salaam


Kutokana na kampuni  ya TBL Group kuonyesha mafanikio ya kuwa mwekezaji bora nchini na mchango wake kutambuliwa na taasisi mbalimbali kwa kuitunukia tuzo ,imekuwa kivutio kikubwa kwa taasisi zinazotaka kupata mafanikio  kwa kutembelea viwanda vyake kwa ajili ya kupata mafunzo na uzoefu na kujua siri ya mafanikio.

Wanachama wa Chama cha Waajiri nchini (ATE) wamefanya ziara katika kiwanda cha TBL cha Ilala ambako wamepatiwa mafunzo ya usalama kazini ikiwemo kuona uzalishaji unavyofanyika kiwandani hapo.



Wanachama wa Chama Cha Waajiri Tanzania(ATE) wakimsikiliza kwa makini mtaalam wa upishi wa TBL Group  Castor Masawe, kuhusiana na  uzalishaji wa bia unavyofanyika

Meneja Usalama,Afya na Mazingira wa TBL Group,Renatus Nyanda aliwapatia somo la kanuni za usalama zinazotekelezwa na kampuni hiyo ambazo zinalenga kulinda usalama wa wafanyakazi wanapokuwa kazini na nje ya kazi ikiwemo wageni mbalimbali wanaofika kiwandani hapo.

Wanachama wa Chama cha Waajiri (ATE) wakipewa maelekezo na Meneja usalama ,afya na mazingira wa TBL Group Renatus Nyanda wakati walipotembelea chumba cha maabara cha TBL Ilala jijini Dar es Salaam

Wanachama hao walifurahishwa na mafunzo hao ikiwemo mkakati wa  kampuni hiyo kuendelea kufanya uwekezaji unaozingatia utunzaji wa mazingira,kuchangia kuendeleza uchumi wa taifa,kupunguza tatizo la ajira na kubadilisha maisha ya jamii kuwa bora.
 Baadhi ya wanachama cha Waajiri Nchini (ATE) wakiangalia vikombe vya tuzo mbalimbali ambavyo TBL Group ilishinda

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA