Saturday 18 June 2016

EURO 2016:: ITALIA NAYO YASONGA 16 BORA

Sampdoria's Eder (No 17) - x- is congratulated by Italy team-mate Emanuele Giaccherini
Mshambuliaji wa Italia, Eder akishangilia baada ya kuifungia bao pekee timu yake dakika 88 ikiilaza 1-0 Sweden katika mchezo wa Kundi E Euro Uwanja wa Manispaaa mjini Toulouse, Ufaransa

ITALIA imefuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya Euro 2016 baada ya kuibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Sweden katika uwanja wa Stade de Toulouse.

Eder - who is currently on a two-year loan at Inter Milan - bends his winning shot into the bottom right corner of the net
Mshambuliaji mwenye asili ya Brazil Eder ndiye aliyefunga goli la ushindi dakika ya 88 baada ya kupokea pasi safi toka kwa Simon Zaza na kupiga shuti kali lililomshinda mlinda mlango.

Mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic ameshindwa kuisaidia Sweden kupata ushindi baada ya kufanya majaribio kadhaa langoni mwa Azzuri lakini ulinzi uliokuwa chini Georgio Chellin ulikuwa imara zaidi.
The big Swede missed with a couple of headers and then put the ball over from a yard out, although he was offside on that occasion
Ibrahimovic akiwa katika hali ya kukata tamaa mara baada ya kila walilofanya kupata bao katika mchezo huo kushindikana
Italia inaongoza kundi E ikiwa na alama sita ikifuatiwa na Ireland ya kaskazini yenye alama moja sawa Sweden huku Ubelgiji ikiburuza mkia kwa kutovuna alama yoyote.

Kesho Ireland ya kaskazini itamenyana na Ubelgiji katika mchezo wa kundi E ili kila timu kuwa sawa katika idadi ya michezo.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA