Wednesday 27 July 2016

CHIDI BENZ: MR BLUE HAKUWAHI KUNITENGA KATIKA SHIDA YANGU


Akiongea kwenye kipindi cha The Playlist cha Times FM wiki iliyopita, Chidi alisema kuwa Blue ni rapper aliyemsaidia bila kuchoka na anamchukulia kama mdogo wake special.Kwa mujibu wa Chidi Benz, watu wote walikuwa na uwezo wa kumwacha na kumchoka katika majaribu aliyoyapitia, lakini si Mr Blue.
Amedai kuwa mara nyingi alikuwa akikutana naye na kuanza kulia kwa jinsi alivyokuwa amedhoofika. “Ila tukikutana naye sasa anaweza akaongea mara akaanza kulia hicho ndicho alikuwa ananiboa,” alisema rapper huyo.
Amedai kuwa Blue alikuwa akitumia muda mwingi kumpa ushauri bila kuchoka.
“Hata kesho he is there for me, he is my young brother, I respect him, I salute him, I am there for him too, whatever he needs I provide,” alisisitiza rapper huyo.
Kwa upande wa Diamond, Chidi amedai kuwa naye amemfanyia mambo mengi makubwa ikiwemo kumlipia takriban milioni 27 kwaajili ya gharama za hospitali kumsaidia aachane na madawa ya kulevya.
“He did it like two times, three times, mpaka akafikia time akawa anakasirika sasa ndio maana this time he is happy, nipo hapo WCB narekodi nyimbo, he is happy.”
Chidi ameachia wimbo wake mpya ‘Chuma’ aliomshirikisha msanii wa WCB, Raymond.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA