Wednesday 20 July 2016

KAMPENI YA NUNUA, UZA, SHINDA NA KONYAGI YAZINDULIWA JIJINI MBEYA


Meneja masoko na Udhamini wa TBL Group,George Kavishe  akizungumza na wadau na wasambazaji (hawapo) wa vileo aina ya konyagi kwenye ukumbi wa Hotel ya Beaco Jijini Mbeya


Baadhi ya wasambazaji kutoka mikoa ya Nyanda za Juu Kusini walishiriki uzinduzi wa Kampeni ya Nunua, Uza Shinda ya Konyagi kwenye Hotel ya Beaco Jijini Mbeya


Mawakala 2 kujishindia lori la tani 3
 Kampuni ya Tanzania Distilleriers Limited (TDL) inayotengeneza na kusambaza kinywaji maarufu cha Konyagi na jamii zake,  imezindua  kampeni ya NUNUA, UZA, SHINDA NA KONYAGI kwa wasambazaji wa bidhaa zake kanda ya Kaskazini.

Kampeni hii inawahusisha wasambazaji wa bidhaa za TDL nchini kote ilizinduliwa rasmi wiki iliyopita jijini Dar es Salaam na  itadumu kwa muda wa wiki 12.

Kanda hiyo ya mauzo inajumuisha mikoa ya Arusha,Manyara,Kilimanjaro na Tanga
Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni hiyo iliyofanyika katika Hotel ya  Kibo Palace mjini Arusha mwishoni mwa  wiki, Meneja Masoko na Udhamini wa TBL Group,George Kavishe  alisema “Dhumuni kuu la kampuni yetu ya TDL kuzindua kampeni ni kwanza kabisa kuwainua wasambazaji wa biashara zetu. Tutaweza kufikia lengo hili kwani washindi wa kampeni hii watajishidia magari mapya mawili ya usambazaji (Eicher 3 Tonne Truck). Tunaamini kwa magari haya wasambazaji wetu wataweza kurahisishwa utendaji wao ndani ya maeneo yao ya mauzo”


Pia, kupitia shindano hili tutaweza kuchangia maendeleo ya kichumi nchini pamoja na jamii kwa ujumla. Aliendelea kusema.


Bwana  Kavishe alisema katika shindano hili  wasambazaji wa bidhaa za TDL wamewekewa viwango vya mauzo; na washiriki wote watakaofikia vigezo wataingia kwenye droo kubwa ya kupata mshindi itakayofanyika mwanzoni mwa mwezi wa 10. “Tunaamini kabisa kampeni hii itaongeza ufanisi kwa wasambazaji wetu nao wataongezea chachu ya manunuzi ya bidhaa zetu”.
Wafanyakazi wa TBL Group katika picha ya pamoja wakati wa uzinduzi huo

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA