MTALII MPANDA MLIMA KUTOKA AFRIKA KUSINI AFARIKI KILIMANJARO
Gugu Zulu akiwa na mke wake |
Mmoja wa watalii wapanda Mlima Kilimanjaro katika msafara maalum wa Afrika Kusini ujulikanoa kama Trek4Mandela, aitwae Gugu Zulu amepoteza maisha yake wakati akipanda kileleni mwa Mlima huo leo asubuhi.
Gugu ambaye ni mtu maarufu nchini Afrika Kusini pia ni dereva wa mbio za magari alikuwa ameambatana na mkewe Letshengo katika msafara huo ambao huandaliwa na taasisi ya Nelson Mandela.
Taarifa zilizotolewa zinaeleza kuwa Gugu alipata matatizo ya kushindwa kupumua, ambapo timu ya matibabu walimwekea dripu na kushuka naye chini ya Mlima, na walijaribu kila wawezalo kuokoa maisha yake lakini ikashindikana.
Marehemu Gugu Zulu akiwa na mkewe Letshengo pamoja na mtoto wao
0 comments:
Post a Comment