Tuesday 19 July 2016

MTALII MPANDA MLIMA KUTOKA AFRIKA KUSINI AFARIKI KILIMANJARO

13671074_629992640496712_1340263080_n
Gugu Zulu akiwa na mke wake
Mmoja wa watalii wapanda Mlima Kilimanjaro katika msafara maalum wa Afrika Kusini ujulikanoa kama Trek4Mandela, aitwae Gugu Zulu amepoteza maisha yake wakati akipanda kileleni mwa Mlima huo leo asubuhi.

Gugu ambaye ni mtu maarufu nchini Afrika Kusini pia ni dereva wa mbio za magari alikuwa ameambatana na mkewe Letshengo katika msafara huo ambao huandaliwa na taasisi ya Nelson Mandela.

Taarifa zilizotolewa zinaeleza kuwa Gugu alipata matatizo ya kushindwa kupumua, ambapo timu ya matibabu walimwekea dripu na kushuka naye chini ya Mlima, na walijaribu kila wawezalo kuokoa maisha yake lakini ikashindikana.

Hii ni mara ya pili kwa watalii wa Afrika Kusini kupanda Mlima Kilimanjaro kwa ajili ya kuenzi juhudi za Mandela katika kuwasaidia watoto wa kike kupitia kampeni maalum ya kupanda Mlima.
                 Marehemu Gugu Zulu akiwa na mkewe Letshengo pamoja na mtoto wao

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA