Friday 21 March 2014

RAIA WAENDELEA KUUWAWA SUDAN

    Askari wa Sudan
    Askari wa kikosi cha Sudan katika jimbo la Darfur
    Shirika la haki za binadamu Human Rights Watch linasema makumi kadhaa ya watu waliuawa katika ghasia zinazoendelea katika jimbo la Darfur nchini Sudan.
    Shirika hilo linasema viongozi wa kijamii katika vijiji viwili wametoa orodha ya majina ya raia takriban arobaini waliouawa katika wiki chache zilizopita kwenye makabiliano baina ya vikosi vinavyounga mkono serikali na vile vya waasi.
    Human Rights Watch linasema wanavijiji wengine makumi kadhaa walishambuliwa, baadhi yao wakipigwa na makombora ya ndege za kijeshi. Shirika la msalaba mwekundu limesema mmoja wa wafanyakazi wake aliuawa jana.
    Umoja wa Mataifa unasema mwaka huu pekee zaidi ya watu laki mbili wameyakimbia makazi yao jimboni Darfur.
    BBC

    0 comments:

    Post a Comment

    OFFICIAL MEMBER

    OFFICIAL MEMBER

    Please Share This Site

    HABARI ZETU

    LIKE PAGE YETU HAPA