Monday 18 July 2016

MTU MWENYE SILAHA AUWA POLISI WATATU HUKO BATON ROUGE MAREKANI


Maafisa polisi watatu wameuwawa kati ya sita waliopigwa risasi na mtu mwenye bunduki aliyefunika sura yake, huko Baton Rouge Marekani, ikiwa ni chini ya wiki mbili tangu kuuwawa kwa mtu mweusi Alton Sterling katika mji huo huo wa Lousiana.

Mwanaume aliyekuwa amevalia mavazi meusi alifyatua risasi hovyo majira ya saa tatu asubuhi, akiwa anatembea katika eneo la duka na eneo la kuogeshea magari kwa mujibu wa mashahidi wa tukio hilo.

Polisi waliarifiwa kwa simu ya 911 kuhusiana na kuonekana mtu anayeranda na silaha eneo hilo, na inaaminika mtu mmoja aliyekuwa na silaha aliwafyatulia risasi polisi walipowasili.

Polisi wamesema mtuhumiwa mmoja mwenye silaha amepigwa risasi na kufa na kuongeza kuwa watuhumiwa wengine wawili hawajulikani walipokimbilia baada ya kushambuliwa na polisi.
               Polisi wakiwa katika hali ya taharuki baada ya wenzao kuuwawa huko Baton Rouge
PICHA NA REUTERS

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA