Monday 18 July 2016

SEHEMU YA PILI::NAMNA YA KUONDOA MSONGO WA MAWAZO NA MFADHAIKO

msongo wa mawazo
Visababishi Vya Msongo Wa mawazo
Kuna vitu vingi vya kimazingira au kimsukumo vinavyoweza kusababisha uwe na msongo wa mawazo, vitu hivi hutwa “stressors”. Nafikiri msomaji wangu unafikiri kuwa kila kitu kinachokuletea msongo wa mawazo (Stressor) ni kibaya, kama kubanwa sana na kazi au mahusiano mabaya ya kimapenzi. Stressor ni kitu cho chote kinachodai matumizi ya juu ya uwezo na nguvu zako za mwili. Inawezekana kuwa kikawa kitu kizuri tu, kama kuoa/kuolewa, kununua nyumba, kujiandaa kwenda chuoni au hata kupandishwa cheo kazini.
Msongo wa mawazo unaweza kutokana na fikra zako binafsi mbali na sababu hizo ambazo ni za nje ye mwili wako. Unaweza kuwa na msongo wa mawazo kutokana na kukifikiria na kukiogopa kitu ambacho kinaweza kutokea au ambacho hakiwezi kutokea au tu ukawa na mawazo chanya kuhusu maisha.
Ni kitu gani kitakupa msongo wa mawazo na kipi hakitakusumbua inategemea sana na namna wewe mwenyewe binafsi utakavyokichukulia kitu kilicho mbele yako, kitu hicho hicho ambacho wewe kinakusumbua, kinaweza kuwa ni burudani kwa mtu mwingine. Kuendesha gari katika foleni toka Mbezi kuingia kazini kwako Posta kunaweza kuwa kero kubwa kwako, wakati kwa  mwingine ni fursa yake ya kupata muziki mwororo asubuhi.
Vitu ambavyo vinasababisha msongo wa mawazo ni pamoj na:
·         Mabadiliko ya maisha
·         Kazi au shule
·         Matatizo katika mahusiano
·         Matatizo ya kifedha
·         Kubanwa na shughuli nyingi
·         Watoto na familia
·         Wasiwasi wa muda mrefu
·         Tabia ya kuona kila kitu ni kibaya
·         Kupenda yasiyowezekana
·         Kutaka kila kitu kiwe sahihi (kikae juu ya mstari) kila wakati
·         Kutopenda kushauriwa au kubadilika kutokana na hali halisi
·         Kujidharau mwenyewe kwenye mazungumzo
Msongo wa mawazo unaotokana na majibizano na rafiki yako, au ule unaotokana na msongamano wa magari au wa kuwa na ratiba ndefu na ngumu ya shughuli ni tofauti na msongo wa mawazo wa kuwa na majukumu mengi katika familia. Msongo wa mawazo unaokwenda kwa muda mrefu ni hatari kwa afya na huweza kuvuruga vitu vingi katika mwili wako ukaishia na magonjwa kama ya high blood pressure, upungufu wa kinga za mwili, kiharusi, ukosefu wa uwezo wa kuzaa au kuzalisha na kuzeeka haraka. Msongo wa mawazo wa muda mrefu huweza kusababisha mfadhaiko (Depression).
USIKOSE SEHEMU YA TATU

KAMA ULIMISS SEHEMU YA KWANZA >>BOFYA HAPA<<

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA