Friday 1 July 2016

UMOJA WA KIJAMII (UKI) CHUO CHA SMMUCo WATEMBELEA KITUO CHA KULEA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM CHA KILIMANJARO ORPHANAGE CENTRE



Baadhi ya watoto wanaoishi na kulelewa katika kituo cha Kilimanjaro Orphanage Centre

Wanaumoja wakiwa katika picha ya pamoja katika lango kuu la kuingia chuoni hapo kwa kampasi ya mjini kabla ya kuelekea kituoni
Umoja wa Kijamii (UKI) ulioanzishwa na wanafunzi wa chuo kikuu cha Stefano Moshi Memorial University wenye lengo la kuitumikia jamii kwa kujitolea kupunguza changamoto za ukali wa maisha katika jamii ulipata fursa ya kukitembelea kituo cha kulea watoto yatima na wenye mahitaji maalum cha Kilimanjaro Orphanage Centre kilichopo kata ya Pasua wilaya ya Moshi mjini  mkoa wa Kilimanjaro.

Akizungumzia historia yao, Mkurugenzi wa kituo hicho Bw. Lazaro Edward alisema kituo hicho kinachopokea watoto kuanzia umri wa miaka mitatu na kuendelea kwasasa kinalea  watoto wapatao 79 huku watano kati yao wakiwa ni waathirika wa virusi vya Ukimwi  kueleza kuwa changamoto kubwa inayowakabili ni idadi ya vitanda pamoja  udogo wa eneo lakini wanatarajia kukihamisha kituo hicho baada ya ujenzi wa kituo rasmi kukamilika.



Wana UKI wakikaribishwa na kupewa maelezo ya awali kutoka kwa Mkurugenzi wa kituo hicho Bw.Lazaro Edward mara tu walipowasili 


Wanaumoja wa UKI wanaosoma kozi mbali mbali walikuwa na wasaha mzuri wa kucheza , kuongea pamoja na kuwakabidhi zawadi watoto hao zenye thamani ya shilingi laki tatu.

Akieleza lengo la kukitembelea kituo hicho mwenyeketi wa umoja huo Bw. Msiyaki Kuruchumila mwanafunzi wa Elimu na Usimamizi wa Bishara alisema kuwa hii ni sehemu ya muendelezo wa  majukumu yao kama Umoja wa Kijamii na hivyo bado safari yao kuelekea kujitoa kwa jamii bado ni ndefu.

Mwandishi wetu alipotaka kujua kwanini kuhusu umoja huu kuwa umejikita zaidi katika chuo cha SMMUCo na je yapo malengo zaidi ya kuutanua,Bw. Kuruchumila alisema kuwa wapo katika mchakato wa kuuneza katika vyuo vyote katika mkoa wa Kilimajaro na wanajitahidi hili liwe limekamilika kabla ya mwezi wa kumi na moja mwaka huu. "Sisi kama SMMUCo peke yetu hatuwezi kwa kuwa jamii inamahitaji mengi na baada ya kuridhika kuhusu uimara wetu ndani ya SMMUCo tumeanza mchakato kuhakikisha UKI inasambaa katika vyuo vyote hapa Moshi ikiwa ni MOCu, KCMC,MWECAU na MWEKA" alihitimisha.


Wana UKI wakicheza na watoto wa Kilimanjaro Orphanage Centre
Watoto wakiteta jambo huku nyuso zao zikiwa na tabasamu la kutembelewa na wageni
Kulia ni mwenyeketi wa UKI Bw. Msiyaki Kuruchumila akikabidhi zawadi kwa watoto hao
Mwenyekiti wa vijana CCM mkoa wa Kilimanjaro Juma Raibu (Kushoto) akiwa na Rais wa Serikali ya wanafunzi SMMUCo Edgar Nziku ambao wote  ni wana UKI wakiwa na watoto kituoni hapo
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA 

Akizungumzia ziara hiyo mmoja kati ya wanaumoja huo Godilisten Mnuo alisema kuwa amejifunza mambo mengi hasa upendo kutoka kwa watoto hao na kutoa wito kwa wadau mbali mbali kuwa na tamaduni ya kudumisha uhusiano na wenye mahitaji kwa moyo wa dhati katika jamii ili kwani hii ndio sifa bora machoni pa Mungu na wanadamu.

Mwana UKI Bw.Said  akiwasimulia hadithi watoto 
WanaUKI wakiwa wameketi na watoto hao huku wakifuatila masimulizi ya hadithi
Wana UKI wakigawa zawadi kwa watoto 
Blogger na muandishi wa mtandao wa Funguka Live  Dickson Mulashani ambaye pia ni mwanaumoja wa UKI  akifurahia jambo pamoja na watoto hao


Mtoto akipatiwa "juice" na mwanadada amabaye ni mwanaUKI

Afisa habari wa umoja huo Bw. Michael akifuatilia moja hadithi
Baadhi ya kina dada ambao ni wana UKI wakikagua sehemu ya malazi kwa watoto kituoni hapo
Rais wa Serikali ya wanafunzi SMMUCo Edgar Nziku akizungumza na mmoja wa watoto kituoni hapo

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA