Tuesday 26 July 2016

WATU WAWILI WAUWAWA KATIKA TUKIO LA SHAMBULIZI LA RISASI HUKO FLORIDA


Watu wawili wameuwawa na wengine 16 kujeruhiwa katika tukio la shambulizi la risasi kwenye klabu ya usiku katika mji wa Fort Myers huko Florida, Marekani.

Shambulizi hilo limetokea kwenye Klabu ya Blu, ambayo ilikuwa ikifanya sherehe kwa kundi la vijana wenye umri mdogo.

Jeshi la polisi linawashikilia watu watatu, na kusema kuwa tukio hilo halina uhusiano na tukio la ugaidi.
   Watu wakiangua vilio katika eneo la Klabu Blu, kufuati tukio la shambulizi la kutumia risasi
                                           Kioo cha gari kilichovunjika baada ya risasi kupenya

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA