Monday 26 September 2016

UMBALI USIWE TATIZO:::FANYA HIVI ILI KUHAKIKISHA MAHUSIANO YENU YANAKUWA IMARA SANA


Usipomuona mpenzi wako kwa muda moyo huingia upweke, matamanio ya kutaka kumuona huongezeka mara dufu, mawazo ya jinsi alivyo na kila kitu kuhusu yeye hukufanya utabasamu na kufurahia uwepo wake kila umuonapo, na hukupa hisia na tamaa ya kutaka kumuona zaidi na kukufanya hitajio la kuwa naye kukuwa na hamasa zako juu yake kuongezeka na kumpenda zaidi.
Vivyo hivyo iwapo muda mrefu ukipita bila kumuona mpenzi wako upweke huzidi na moyo huchoka, hamasa na taamaa zinabadilika kuwa mzigo, mawazo mazuri ya kimapenzi na husuda hubadilika kuwa msongo, njisi muda unavyozidi kwenda na ndivyo hamasa ya mpenzi wako ndivyo inavyoisha na kuzidi kushuka, moyo unasahau mguso wake aliokuwa nao kwako, shauku ya kuongea inapungua, kama mlikua mnaongea kila baada ya masaa mawili kwenye simu, masaa yatabadilika na kuwa matatu, yakiwa matatu yatabadilika kuwa siku nzima, umbali unakuwa tena hautengenezi upweke wa kutaka kuonana bali unawafanya mioyo yenu kusahauliana na umbali wa hisia kati yenu kuongezeka.




Leo nimekuandalia njia tano za kuongeza hamasa na kuondokana na upweke unaosababisha hisia kupungua pamoja na mvunjiko wa mapenzi ndani ya mahusiano ya mapenzi ya umbali, ukitaka mambo yako yaende salama hakikisha unazingatia njia hizi muhimu.

  • Namba 1, Hakikisha unaongea kile kilicho moyoni mwako.

 Wanawake wanauwezo mkubwa wa kugundua iwapo kuna kitu kinakusumbua na vile vile wanawake ni rahisi sana kujihisi, kama wamekugundua umeudhika na usipokielezea mapema akiwa amekuuliza, moja kwa moja ataanza kujifikilia ni yeye ndio aliyesababisha au ni kwa ajiri ya uhusiano kwa sababu yuko mbali unakuwia vigumu ila unakuwa hautaki kuelezea wazi, kwahio kwa mahusiano ya mbali inakubidi uwe mwangalifu na mvumilivu, kama kuna kitu kati yenu hakiendi vizuri, ni vizuri mkakiongea kwa wakati ulio mwafaka, iwapo mkakiacha kikawajengea kinyongo ndani ya mapenzi yenu na kufikia hatua ya kuudhiana, ugonvi wa mapenzi kwa wapenzi walio mbali ni mgumu sana kusuruhishwa.




  •  Namba 2, Hakikisha mnapanga jinsi ya kukutana.

Umuhimu wa kukutana na kuonana ana kwa ana ni mkubwa sana hasa kwa mapenzi ya mbali, kukutana huamsha hisia na mvuto ndani ya mapenzi uliosahaulika, muda ni dawa ya kusahau kwahio iwapo mkiacha kukutana kwa muda mrefu, yale maumivu yanaosababishwa na upweke wa kutomuona mpenzi wako huisha na hamasa za mapenzi pia hupungua, binadamu ameumbwa kubadilika kutokana na mazingira, kwahio mkiruhusu muda mrefu kupita bila kuonana utofauti lazima utaingia kati yenu hata kama mlikua na mapendo makubwa kiasi gani, umuhimu wa kuongea hautokuwepo tena na hisia zitapolomoka na kusababisha mvuto kuisha kabisa ndani ya uhusiano wenu.


  • Namba 3, Fanyeni vitu kwa pamoja mkiwa mbali.

Kwa tekenolojia ilivyongezeka kipindi hichi, hamuhitaji muwe mji au mtaa mmoja ili muweze kufanya kitu cha kuwafurahisha pamoja, tafuteni kitu kipya cha kuongelea iwe filamu au kitu chochote kingine ambacho wote wawili mnafurahia na kupenda kukifanya au kufuatilia, mnaweza pigiana simu na kutaalisha filamu na wote mkaanza kuiangalia kwa wakati mmoja, pande zote mbili mnatakiwa kuwa wabunifu na mapenzi hayatawezekanika iwapo upande mmoja pekee ukiwa unajitahidi wakati mwingine unategea na kutokujali, na kila mkiongea hakikisha hamtumii sana neno nimekumisi, chochote kikiwa kinatamkwa sana na kusikiwa kila siku hupoteza mvuto na kuwa neno la kawaida na kusababisha maongezi kuisha mapema.


  • Namba 4, Tambulishaneni kwa marafiki wapya na jitahidi usiwe na wivu uliopitiliza kwa  marafiki wake wa jinsia tofauti.

Kitu kimoja uhusiano wa mbali unachosababisha ni kutoa muda mwingi wa kutumia na marafiki, kazi yako kama mpenzi wake unatakiwa usionyeshe wivu wako maana utakuona humuamini na kusababisha asikushilikishe kwenye baadhi ya mambo mengine maana anajua iwapo akifanya hivyo hautohafiki na zaidi ya hapo itasababisha ugomvi ambao haupo na itamfanya pia na yeye kuwa na wasi wasi na wewe pia, kujiamini na kutomtilia mashaka mpenzi wako kunatengeneza hali ya kuaminiana na kusababisha uhusiano ujijenge katika hali nzuri ya amani na yenye msimamo zaidi.


Kutambulishana kwa marafiki wapya inawafanya muwe huru na kupata mengi ya kuongea. 


  • Namba 5, Ongeeni kwa kutumia njia za kuonana mara kwa mara.

Tumieni tekenelojia iliyopo kuongeza hamasa, mvuto na chachu ndani ya mapenzi yenu, kuonana ana kwa ana kwa kutumia njia za skype, google talk au kutumiana video kwenye whatsaap kunaleta hali ya uhalisia zaidi na kufanya kusimuliana kuhusu kitu cha kijinga rafiki yako alichokifanya au mfanyakazi mwenzio anavyokuboa kuwe na hali ya mawasiliano yenye mvuto zaidi.


Kuona tena tabasamu lake na jinsi uso wake unapotabasamu kulipua hisia zako maradufu na za kwake pia na kusababisha hamasa na hisia zilizosahaulika kurejea tena kwa mara nyingine.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA