Tuesday 9 November 2021

MBINU SITA (6) SAHIHI ZA KUWEKA AKIBA ZAIDI NA KUWEKEZA VIZURI.


Kuna mambo mengi unayotaka kuyafanikisha katika kipindi hiki cha maisha yako. Bila ya kukanusha ,Ukweli ni kwamba baadhi ya ndoto zako zina gharimu fedha. Na ufunguo wa kuzifanikisha ndoto hizo ni kujifunza kusimamia fedha.

Pale unapokuwa umeshajifunza misingi ya kuhifadhi au kuweka akiba na kuwekeza fedha, bila shaka utaweza kuyafanikisha malengo yako.

Katika uchumi wa sasa wenye uhaba wa nishati na gharama za vyakula kuwa kubwa na kukua kwa kasi ya ukosefu wa ajira, kusimamia fedha kunaweza kukawa ni kazi ngumu sana ,lakini kwa hakika hakuna hata jambo moja lisilowezekana .Unawezaje kwenda na hali hii? Zifuatazo ni mbinu sita za kuweza kuweka akiba fedha nyingi zaidi na kuwekeza vizuri.

1. kuweka bajeti ni kipaumbele
Matumizi ya mara kwa mara na ya muda mmoja, kila aina ya matumizi , hata matumizi ya hiari. kama bajeti yako inahusisha vitu vyote hivyo, kuna uwezekano mkubwa sana wa wewe kutokuwa nje ya fedha, unaweza kusimamia fedha zako kwa kujiwekea bajeti tu. kwa njia hii unaweza kuwekea kipaumbele  matumizi yako  na kupanga fedha zako kwenye vitu vyenye umuhimu mkubwa sana kwenye maisha yako. ni muhimu kuweka na kutoa umakini kwenye vitu vidogo ambavyo vinaweza kuongezeka kwa kiasi kikubwa sana.

Kamwe usivipuuze vidogo vidogo au mambo madogo, hakika najua unataka vyote, lakini weka vipaumbele  kwenye vitu unavyovihitaji kwanza na vipi vya kusubiria kwa ajiri ya baadaye, Na kutumia kutokana na utaratibu huo.

2. Boresha rekodi ya matumizi.
Unahitaji kuangalia kwa makini na kwa karibu sana mahali fedha zako zinapokwenda  na wapi hasa unaweza  kukata pembe. magazeti ,Kunywa kahawa -vitu vyote vinahesabiwa,haijalishi unatumia kiasi kidogo cha pesa, vyote vinaongezeka na kuwa kiasi kikubwa sana, hivyo, unahitaji kufuatilia kila kitu. njia bora na iliyo nzuri ni kudumisha rekodi ya matumizi .jaribu kuandika na kuweka kumbukumbu juu ya vitu unavyotumia kwa zaidi ya mwezi. ukihusisha na kila manunuzi. kama utaweza kufanya hivyo kwa muda mrefu sana, utaweza kupata picha sahihi juu ya wapi hasa unatumia fedha zako na namna gani unaweza  kupunguza na kuweza kukata kabisa  gharama huko.

Katika Kuongeza na hili ,unaweza kugawanya matumizi yako katika makundi mawili; mara kwa mara na yasiyo ya mara kwa mara .hii itakusaidia kuwa na usimamizi wenye nguvu juu ya matumizi yako ya mwezi.

3. Futa madeni yote.
Kama upo kwenye madeni au unapambana kifedha, moja ya  njia rahisi sana kupambana na hali hii kutambaa kwenye magamba yako na kupuuzia nakala yako ya benki na mahitaji ya malipo. lakini hili ,kwa kutokuwa  na maana, inaenda kufanya vitu kuwa rahisi. badala yake ,kabili tatizo, jua unahitaji kushughulika na nini, Na ushakapokuwa  sahihi katika hili, utakuwa na ufahamu wa hatua inayofuata. ni muhimu  madeni yako yawe madogo vyovyote vile unavyoweza bila ya kuikabili biashara yako.

4.  Bima ni hatua ya kwanza.
Moja ya hatua ya msingi kwa ajiri yako na kwa familia yako hapo baadaye ni bima. kuna aina kadhaa za bima kama vile bima ya afya, bima ya ulemavu, bima ya umiliki wa nyumba.

5.  Anzisha lengo la kuweka akiba na weka akiba mara kwa mara.
Jitazame kwenye kioo na Kisha na useme hivi- Mwisho wa mwezi huu, utaweza kununua gari ya ndoto yako kutoka kwenye akiba yako, Moja ambayo umekuwa ukiisubiri mno kwa muda wote huo hii inakufanya hujisikiaje? msisimko? hakika! hii, kwa vyovyote vile ,haitoweza kuwa kweli mpaka pale utakapokuwa na busara na kuanza kuweka akiba fedha zako ili kufanikisha lengo lako. Jambo unalotakiwa kuliweka akilini mwako pale unapokuwa unaweka akiba fedha yako ,Ni kuweka umakini juu ya nini utaweza kufanya baada ya kuweza kufanikiwa kuweka  fedha nyingi ,Ni muhimu kujua hizo fedha unazoziwekea akiba utazitumia kwa ajiri ya nini, Utazifanyia nini? kuliko kufikiria tu kuweka fedha zako pembeni.

Ni muhimu kuwa na malengo ya kujiwekea akiba fedha zako. lakini watu wengi hawajui jinsi ya kuweka akiba fedha zao, kwa hiyo, Unataka kuweka akiba ya fedha mara kwa mara lakini haujui cha kufanya? Kama umeajiriwa;

Ingia akaunti ya kuweka akiba.
Weka maelekezo yenye msimamo, ili kila mwezi fedha yako iweze kupata kusafirishwa kwenye akaunti yako ya akiba moja kwa moja bila ya wewe kuwa na hofu kuhusu fedha yako. Na kamwe usisubiri mpaka mwisho wa mwezi kwa ajiri ya hili. Kwani kuna faida tatu za kufanya hivyo;

1.Fedha inapata kusafirishwa kwenye akaunti yako ya akiba mapema sana pale unapolipwa mshahara wako, kama umeajiriwa.

2. Kiasi ulichoweka akiba kitaongezeka ikiwa utapata ongezeko la mshahara na pia utapata Marejesho ya kiasi  ushindani juu ya akiba yako.

6. Tathimini uvumilivu wako wa hatari.
Hatari inafanya  kazi kubwa sana, Na ya muhimu kwenye kufanya maamuzi yote ya uwekezaji. kanuni ya shaba ni Inasema kwamba ,Kadri marejesho yanavyokuwa makubwa kutoka kwenye baadhi ya Sehemu za  uwekezaji, Ndiyo hatari inavyoweza kuhusika kwa ukubwa zaidi. Baadhi ya sababu muhimu zinaoweza kukusaidia kuamua uvumilivu wako wa hatari ni  kama vile Mapato, matumizi, malengo yako ya kifedha n.k.

kama unataka kufanya maamuzi yenye busara Au Yenye hekima kwenye uwekezaji, Unahitaji kutathimini uvumilivu wako wa hatari kabla ya kujiingiza kwenye kitu chochote kile.

Moja ya kitu kigumu sana kuhusu kusimamia na kuweka akiba fedha Ni hatua ya kwanza sana -kuanza. hii inaweza kuwa ni vigumu sana kutumia akiba yako kwa busara ili kuelekea kwenye malengo yako ya kifedha .
Mbinu zilizotajwa hapo juu zitakusaidia kwa kiasi kikubwa sana kuendeleza mpango wa ukweli wa kuweka akiba na kuwekeza. zaidi ya hapo, Zitakusaidia kuelewa mambo yanayohusiana na fedha kwa njia bora zaidi. Zifuate Mbinu hizo na hakuna lolote lile litakalokuzuia kuweza kufanikisha mafanikio ya kifedha. TUPO PAMOJA.
Geofrey Mwakatika

Mwakatikageofrey@gmail.com.  0767382324.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA