HISPANIA YAIBADILISHIA UINGEREZA "GIA" NA KULAZIMISHA SARE (2-2)
ENGLAND imeporwa tonge kinywani katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Hispania. Kocha mpya wa England, Gareth Southgate alishuhudia timu yake ikiongoza 2-0 hadi dakika ya 88 lakini hadi mwisho wa mchezo matokeo yakawa 2-2.
Adam Lallana aliifungia England bao la kwanza kwa mkwaju wa penalti dakika ya 9 kabla ya Jamie Vardy kupachika la pili dakika ya 48, hilo likiwa bao lake la kwanza baada ya kucheza kwa dakika 937 bila bao kwa klabu yake ya Leicester City na England.
Hispania wakachomoa bao moja dakika ya 89 kupitia kwa Iago Aspas huku Isco akisawazisha katika dakika ya za majeruhi.
0 comments:
Post a Comment