Tuesday 27 December 2016

LIGI KUU UINGEREZA::MAN UNITED YAPATA USHINDI WA NNE MFULULIZO

Henrikh Mkhitaryan calls his scorpion kick goal 'my best ever' as he revels in 'Christmas

  Mchezaji raia wa Armenia Henrikh Mkhitaryan akifunga goli kwa kisigino

Manchester United imepata ushindi wa nne mfululizo wa Ligi Kuu ya Uingereza katika mchezo walioutawala dhidi ya Sunderland inayobakia katika mstari wa kushuka daraja baada ya kulala kwa magoli 3-1.

Manchester United iliyostahili ushindi iliutawala mchezo huo kwa asilimia 63, ilipiga mashuti 25 kwenye goli, lakini zilikuwa jitihada za beki Daley Blind zilizozaa matunda na kuipatia goli la kwanza kufuatia pasi ya Zlatan Ibrahimovic.

Katika kipindi cha pili Zlatan Ibrahimovic aliongeza goli la pili akinasa pasi ya Paul Pogba huku Henrikh Mkhitaryan aliyetokea benchi akifunga goli la kisigino licha ya kuonekana ameotea.
                     Zlatan Ibrahimovic akianza kushangilia goli wakati mpira ukielekea wavuni

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA