Monday 5 June 2017

KIKOSI CHA TAIFA STARS CHAENDELEA KUJINOA NCHINI MISRI

MIS2

Kipa Said Mohammed Nduda , akichupa kuzuia mpira wakati wa mazoezi yanayosimamiwa na Kocha wa Makipa wa Taifa Stars, Patrick Mwangata aliyepiga magoti katika mazoezi yanayofanyika Kituo cha michezo cha Tolip (Tolip Sports City) hapa Alexandria, Misri. 

Taifa Stars inayodhaminiwa na Bia ya Serengeti inayozalishwa na Kampuni ya Bia ya SBL, inajiandaa kucheza na Lesotho Juni 10, 2017 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataiafa ya Afrika (AFCON) za mwaka 2019 zitakazofanyika Cameroon.
MIS3
Kiungo wa pembeni wa Taifa Stars, Simon Msuva akiwa kwenye kasi kuwahi mpira wakati wa mazoezi ya timu hiyo yanayofanyika Kituo cha michezo cha Tolip (Tolip Sports City) hapa Alexandria, Misri.
 
MIS4
Libero wa Taifa Stars, Erasto Nyoni (katikati) akijitahidi kudhibiti mpira mbele ya washambuliaji wenye njaa ya kufunga, Ibrahim Ajib (kulia) na Abderheman Mussa kabla ya kipa Said Mohammed hajatokea kusaidia wakati wa mazoezi ya timu hiyo yanayofanyika Kituo cha michezo cha Tolip (Tolip Sports City) hapa Alexandria, Misri. 

 Picha na Alfred Lucas wa TFF.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA