Wednesday, 14 May 2014

Ehud Olmert jela kwa miaka sita


120105105947_jp_olmert304x171_nocredit_16eb6.jpg
Ehud Olmert

Mahakama moja nchini Israel imempa kifungo cha miaka sita jela aliyekuwa waziri mkuu nchini Israel Ehud Olmert kwa kosa la kupokea hongo.
Bwana Olmert alipatikana na hatia mwezi machi katika kile kilichojulikana kama 'swala la eneo takatifu' ambapo hongo ilitolewa ili kuharakisha ujenzi wa majumba ya kifahari mjini Jerusalem.
Kiongozi huyo alikuwa ameondolewa mashitaka katika kesi tofauti zilizokuwa zikimkabili.
Mashitaka yaliomkabili yalitekelezwa wakati Olmert alipokuwa meya wa mji wa Jerusalem na baadaye akiwa waziri wa serikali.
Ehud Olmert alimrithi Ariel Sharon kama waziri mkuu mnamo mwaka 2006 baada ya Sharon kuugua ugonjwa wa kiharusi.
Alijiuzulu mnamo mwaka 2008
.CHANZO BBC,(A.I)

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA