AIBU: WATU WANNE WA FAMILIA MOJA WAKAMATWA WAKILIMA SHAMBA WAKIWA UCHI
09:11 |
No Comments |
Jeshi la polisi Mkoani Simiyu linawashikilia watu wanne wa familia
moja kwa tuhuma ya kukutwa wakilima uchi wa mnyama shambani kwa kile
kinachodaiwa kuwa ni imani za kishirikina.
Kaimu kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Simiyu Venansi Kimario
alisema tukio hilo limetokea septemba 2 majira ya saa 12 asubuhi
katika kijiji cha Bushikwamala kata ya Kalemela wilayani Busega Mkoani
Simiyu
Kimario alisema kuwa watu hao walikamatwa na jeshi la polisi alfajiri
huko Bushigwamhala wakiwa wanalima kwenye shamba lao na walipohojiwa
walidai kuwa walielekezwa na babu yao kipindi cha uhai wake kuwa
wakilima uchi watapata mavuno mengi.
Kamanda Kimario aliwataja waliokamatwa kuwa ni Makoye Kagoje (42), na mke
wake Neema Kigwela (31) pamoja na watoto wao, mmoja wa kiume (15) na
wa kike (12) majina yamehifadhiwa.
Aidha Kimario alisema watu hao pamoja na watoto wao wanashikiliwa na
jeshi la polisi kwa kukutwa wakifanya vitendo vya ushirikina.
Babu yao alishafariki mwaka jana na aliwaambia kuwa wakilima wapo uchi
watapata mavuno mengi, hivyo waliamua kufanya hivyo kutokana na wosia
wa babu yao
Alisema baada ya jeshi la polisi kupata taarifa kutoka kwa raia wema
liliweza kufika katika eneo hilo na kuwakamata watuhumiwa hao wakiwa
wanaendelea kulima bila nguo.
Hata hivyo Kimario amewataka watu wasijishirikishe kwenye
vitendo vya ushirikina na siyo kwamba ukilima uchi utapata mazao mengi
tofauti na kufuata kanuni za kilimo bora, viongozi wa madhehebu ya
dini na viongozi wa serikali tuwaelimishe watu waachane na imani za
kishikina .
EDDY BLOG
Na Faustine Fabian-Simiyu
Related Posts:
MVUA KUBWA YASABABISHA MAFURIKO KATIKA MIJI KADHAA UINGEREZA,MECHI YA UEFA YALAZIMIKA KUAHIRISHWA Miji ya Manchester na Lancashire nchini Uingereza imekumbwa na mvua kubwa, iliyosababisha mafuriko na umeme kukatika huku mvua ya kimbun… Read More
PROF. MBARAWA ATOA MIEZI SITA KUMALIZA UPANUZI WA UWANJA WA NDEGE WA MWANZA Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa mkandarasi Nyanza Road Construction inayojenga barabara ya Fu… Read More
WASHIRIKI 10 WAINGIA FAINALI KATIKA SHINDANO LA GOSPEL STAR SEARCH 2016 JIJINI DAR Kikundi cha Makerubi kutoka Manyara ambao walijiandikisha wakitokea Temeke waliweza kufanikiwa kuingia hatua ya nusu fainali katika shindano la Go… Read More
UEFA:::ARSENAL YAIKOMALIA PSG UGENINI Alexis Sanchez akijipinda na kuachia shuti lililosawazisha goli Alexis Sanchez ameisaidia Arsenal kuambulia pointi moja katika Li… Read More
SHULE ZA FEZA KUFUNGUA TAWI LAKE MKOANI MWANZA. Kutoka kushoto ni balozi wa shule hizo mkoani Mwanza, Faisal Hafidh na Taasisi ya Time To Help, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza n… Read More
0 comments:
Post a Comment