HAHA NOMAA :CHEKI VIDEO YA KILICHOMTOKEA SIMBA AKILA MZOGA WA KIBOKO
Mnyama anapokufa, vitu vilivyopo tumboni huwa vya kwanza kuanza kuoza na kusababisha mkusanyiko wa gesi. Wingi wa gesi hiyo mara nyingi husababisha mzoga kuvimba, kama gesi haina njia ya kutoka nje. Mpasuko wa mzoga huo husababisha “mlipuko” kutokana na shinikizo (pressure) linalosababishwa na mkusanyiko wa gesi. Na hicho ndio kilichotokea wakati Simba huyu akijaribu kula mzoga wa kiboko.
