Monday 24 November 2014

MKUU WA WILAYA AAGIZA WANAFUNZI 24 WALIOPATA MIMBA WARIPOTI POLISI



http://i1.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2014/11/news-12.jpg
Mkuu wa Wilaya ya Rufiji  Mkoani Pwani,Nurdin Babu  ameagiza wanafunzi24 wa Sekondari mbalimbali Wilayani humo waliopata ujauzito kuripoti kituo cha polisi November25 mwaka huu ili wasaidie kutoa ushirikiano wa kuwakamata wahusika waliowapa mimba na kuweze kukamatwa.

Sambamba  na wanafunzi hao pia wazazi au walezi wa wanafunzi hao  wametakiwa kuripoti wakiwa na watoto wao ambapo atazungumza na wazazi pamoja na wanafunzi hao ili kujua tatizo ni nini.

Babu alisema taarifa za watoto 26 walipata ujauzito katika kipindi cha Januari hadi Oktoba si nzuri na lazima hatua za kinidhamu zichukuliwe ili kuondokana na matatizo hayo ndani ya jamii.

Alisema idadi ya wanafunzi waliokatishiwa masomo ni kubwa na Serikali haiwezi kulifumbia macho suala hilo.
-EDDYBLOG

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA