MKUU WA WILAYA AAGIZA WANAFUNZI 24 WALIOPATA MIMBA WARIPOTI POLISI
09:30 |
Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani,Nurdin Babu ameagiza wanafunzi24 wa Sekondari mbalimbali Wilayani humo waliopata ujauzito kuripoti kituo cha polisi November25 mwaka huu ili wasaidie kutoa ushirikiano wa kuwakamata wahusika waliowapa mimba na kuweze kukamatwa.
Sambamba na wanafunzi hao pia wazazi au walezi wa wanafunzi hao wametakiwa kuripoti wakiwa na watoto wao ambapo atazungumza na wazazi pamoja na wanafunzi hao ili kujua tatizo ni nini.
Babu alisema taarifa za watoto 26 walipata ujauzito katika kipindi cha Januari hadi Oktoba si nzuri na lazima hatua za kinidhamu zichukuliwe ili kuondokana na matatizo hayo ndani ya jamii.
Alisema idadi ya wanafunzi waliokatishiwa masomo ni kubwa na Serikali haiwezi kulifumbia macho suala hilo.
-EDDYBLOG
Related Posts:
RAIS DKT. MAGUFULI AMTEUA GABRIEL DAQARRO KUWA MRITHI WA GAMBO ARUSHA Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 21 Agosti, 2016 amemteua Bw. Gabriel Fabian Daqarro kuwa Mkuu wa… Read More
RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI AMUAPISHA MKURUGENZI MKUU MPYA WA IDARA YA USALAMA Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.John Pombe magufuli akimuapisha Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt Modestus Francis Kapilimba Ikulu ji… Read More
WANANCHI WAJITOKEZA KUUPOKEA MWENGE WA UHURU JIJINI ARUSHA Mkuu wa wilaya ya Arusha,Gabriel Daqarro akiwa ameshika Mwenge wa Uhuru uliopokelewa leo katika Jiji la Arusha eneo la Kisongo kwaajili ya ku… Read More
PICHA: JESHI LA POLISI LIKIFANYA MAZOEZI YA UTAYARI WA KUKABILIANA NA UHALIFU NA WAHALIFU NCHINI Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia wa wakiwa moja ya maozezi yao ya kupasha viungo kabla ya kuanza mazoezi ya kutuliza ghasia. Askari Polisi … Read More
DK. SHEIN AKUTANA NA MADAKTARI BINGWA KUTOKA HOSPITALI YA CHUO KIKUU CHA EL SHATBY CHA NCHINI MISRI Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Prof.Saber Waheeb,Kiongozi wa Ujumbe wa Madaktari bingw… Read More