UKAGUZI WA VIBALI VYA AJIRA KWA WAGENI KUANZA
Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu
wenye ulemavu), Bibi. Jenista Mhagama (Mb), akifuatilia maelezo ya
wajumbe wa kikosi Maalum cha kukagua vibali vya Ajira za Wageni (hawapo
pichani) wakati alipokutana nao Jijini Dar es Salaam tarehe 29 Desemba,
2015, (katikati) ni Naibu Waziri (Kazi, Ajira na Vijana), Anthony
Mavunde na Katibu Mkuu (kazi na Ajira), Eric Shitindi.
Serikali
imeamua muda wowote kuanzia mwezi huu kuanza ukaguzi wa vibali vya Ajira
za Wageni nchini, kufuatia muda wa siku 14 kuisha uliotolewa na
serikali katika tangazo la utolewaji wa vibali vya kazi kwa wageni
nchini lililotiwa saini Desemba 14, mwaka huu, na Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Aiira, Vijana na Watu wenye
ulemavu), Jenista Mhagama (Mb), ambaye aliwataka waajiri wote nchini kwa
muda wa siku hizo wawe wametekeleza matakwa ya Sheria ya Kuratibu Ajira
za Wageni nchini Na. 1 ya Mwaka 2015.
“Katika
taarifa tuliyoitoa mwezi huu, tuliwajulisha waajiri wote wenye waajiriwa
wageni ambao wana vibali vya kazi za muda (Carry on Temporary
Assignment) na wale wote wasiokuwa na vibali vya ajira vilivyotolewa na
kamishna wa kazi nchini kuwa wanatenda kosa. Kamishna wa kazi amepewa
mamlaka kutoa vibali vya ajira kwa wageni wanaotaka kufanya kazi nchini.
Hivyo hakuna mamlaka nyingine yoyote inayoruhusiwa kutoa vibali vya
ajira kwa wageni,” amesema Mhagama
Amesema
hayo, Tarehe 29 Desemba, 2015, Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza
na kikosi maalum kitakachoendesha operasheni hiyo chenye wajumbe kutoka
Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uhamiaji na Wakala wa Usalama na Afya
mahali pa kazi (OSHA), ikiwa lengo ni kufuatilia kama agizo lililotolewa
na serikali limefuatwa na kuhakikisha taratibu zinazopaswa kufuatwa
katika utoaji wa vibali vya ajira zinazingatiwa.
“Serikali
ilitoa muda wa siku 14 kwa waajiri wote wawe wametekeleza matakwa ya
Sheria Na. 1 ya mwaka 2015 vinginevyo hatua kali za kisheria
zitachukuliwa dhidi yao.” Alisitiza Mhagama.
Mwezi
Machi, mwaka huu Bunge la 10 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
lilipitisha Sheria ya Kuratibu Ajira za Wageni nchini Na. 1 ya Mwaka
2015 (The Non-Citizens (Employment Regulation) Act)). Sheria imeanza
kutumika rasmi tangu tarehe 15 Septemba, 2015. Sheria hiyo inaanzisha
Mamlaka moja yautoajiwa vibali vya ajira kwa wageni na Mamlak ahiyo ni
Kamishna wa Kazi.
0 comments:
Post a Comment