Thursday 5 February 2015

STEVEN GERRARD AFIKISHA MECHI YA 700 AKIITUMIKA LIVERPOOL AVAA KIATU CHA KUMBU KUMBU


KIUNGO Steven Gerrard amekuwa mchezaji wa tatu wa Liverpool kutimiza mechi 700 kihistoria baada ya kuichezea timu hiyo jana ikishinda 2-1 dhidi ya Bolton katika mechi ya marudio Raundi ya Nne ya Kombe la FA.
Nahodha huyo wa Liverpool, alirejeshwa kwenye kikosi cha kwanza na kocha Brendan Rodgers, na kuingia kwenye orodha ya Ian Callaghan na Jamie Carragher walioichezea pia mechi 700 klabu hiyo.
Gerrard, ambaye maisha yae yote amecheza Liverpool tu, alifurahia mafanikio yake hayo kwa kuvaa kiatu maalum kilichoandikwa 700 nyuma pamoja na majina ya mabinti zake, Lilly na Lexie.
Steven Gerrard made his 700th Liverpool appearance on Wednesday night in their game against Bolton
Steven Gerrard amecheza mechi ya 700 Liverpool jana
The boots had the No 700 on the back as well as the name of his daughters Lilly and Lexie
Kiatu alichovaa Nahodha huyo jana, No 700 chenye majina ya mabinti zake pia, Lilly and Lexie

WALIOCHEZA MECHI NYINGI LIVERPOOL

1. Ian Callaghan 857
2. Jamie Carragher 737
3. Steven Gerrard 700*
4. Ray Clemence 665
= Emlyn Hughes 665 
(bado anacheza) 
Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 34 alibandika ujumbe kwenye ukurasa wake wa Instagram wiki iliyopita kuelezea anavyojiandaa kwa mechi ya 700, lakini hakuwemo kwenye kikosi kilichoifunga West Ham 2-0 Uwanja wa Anfield mwishoni mwa wiki.
Gerrard anaweza kubaki nafasi ya tatu kwa kucheza mechi nyingi Liverpool, nyuma ya  Callaghan aliyecheza mara 857 na Carragher michezo 737, kutokana na kuwa na mpango wa kuhamia LA Galaxy ya Marekani akalizie soka yake huko mwishini mwa msimu.


0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA