Saturday 27 June 2015

ZOEZI LA UGAWAJI VYETI KWA WANACHAMA WA MALIHAI CHUO KIKUU CHA KUMBUKUMBU YA STEFANO MOSHI LAFANA

Mwenyekiti wa MALIHAI chuo kikuu cha kumbukumbu ya Stefano Moshi David Kaganda akimkabidhi cheti mwanachama katika campus ya Mwika
Zoezi hilo lililofanyika katika campus mbili tofauti za chuo hicho kilichopo mkoani Kilimanjaro  ikiwa ni Masoka pamoja na Mwika  liliendeshwa na viongozi wa chama hicho cha watunza mazingira nchini Tanzania.

Akisimamia zoezi hilo katika campus  ya Mwika ,mwenyekiti wa MALIHAI chuoni hapo  David Kaganda aliambatana na rais mteule wa chuo hicho  Filbert Mafuta ambapo waligawa vyeti hivyo kwa wanachama wa mwaka wa tatu wanaotarajia kuhitimu masomo mwezi ujao.

Zifuatazo ni picha za tukio hilo katika campus ya Mwika.




Mwenyekiti wa MALIHAI David Kaganda akiwasilisha ripoti fupi ya mwenendo wa Chama mbele ya waliohudhuria zoezi hilo

Wanachama wa MALIHAI campus ya MWIKA waliohudhuria zoezi hilo wakimsikiliza Mwenyekiti wao 
Mwenyekiti wa MALIHAI David Kaganda (wakwanza kushoto) Samwel Mwakeja aneafuata ,Rais wa Serikali ya wanafunzi Filbert Mafuta (aliyevaa Suti) wakiwa katika picha ya pamoja






Wanafunzi waliokabidhiwa vyeti katika picha ya pamoja na viongozi wa MALIHAI
Viongozi wa MALIHAI na wale wa Serikali ya wanafunzi chuoni hapo katika picha ya pamoja
Picha na Abdul Hakim Hilal

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA