RAIS OBAMA AZUNGUMZIA UGAIDI
Rais wa Marekani Barack Obama
Rais
Barack Obama wa Marekani amekubali kutoweka bayana mipango ya serikali
yake katika mapambano dhidi ya ugaidi duniani na hasa kundi la
wanamgambo wa dola ya kiislam maarufu kama Islamic State.
Amesema
kwamba ikiwa watu hawafahamu juu ya maelfu ya mashambulio ya anga
yanayoongozwa na majeshi ya Marekani na washirika wake dhidi ya
wanamgambo hao, basi watakuwa na mashaka kwa kile kilichokwisha fanyika
na kwamba juhudi hizo hazijatosha.
Rais
Obama alitoa tamko hilo katika mahojiano ya wazi yaliyofanywa mwanzoni
mwa wiki hii akiwa mapumzikoni nje ya nchi yake; yeye na familia yake
katika visiwa vya Hawaii.
Rais
Obama hakusita kuelekeza shutuma zake kwa mgombea wa chama cha
Republican anayegombea nafasi ya urais, Donald Trump kwa kuleta
mkanganyiko pamoja na kuzidisha wasiwasi na kuwataka wanaume
waliostaarabika na wenye elimu ya kutosha kuongeza nguvu katika kampeni
za mgombea huyo.
Trump
aliwahi kutoa wito wa kuzuiliwa waisilamu kuingia nchini Marekani baada
ya shambulio la hadhara mjini California lililosababishwa na wapenzi
wawili wanaoaminika kuwa ni watu waliokuwa na msimamo mkali.-BBC
0 comments:
Post a Comment