Tuesday 5 January 2016

Saudi Arabia yawatimua wanadiplomasia wa Iran

Mfalme wa Saudi Salma bin Abdul-Aziz al-Saud.
Mfalme wa Saudi Salma bin Abdul-Aziz al-Saud.
Saudi Arabia imevunja uhusiano wa kidiplomasia na Iran, baada ya waandamanaji kuuvamia ubalozi wake mjini Tehran na kuuchoma moto, na kutoa saa 48 kwa wanadiplomasia wa Iran kuondoa nchini humo.
Hatua ya Saudi Arabia ilikuja saa chache baada ya waandamanaji kuuvamia na kuuchoma moto ubalozi wake mjini Tehran, katika kupinga mauaji ya kiongozi wa Kishia Sheikh Nimr al-Nimr.
Mauaji ya Nimr pamoja na wengine 46 - ambayo ndiyo makubwa zaidi kufanywa kwa wakati mmoja katika kipindi cha miongo mitatu na nusu - yamebainisha wazi migawanyiko mikubwa inayoikabili kanda ya Mashariki ya Kati, ambako waandamanaji waliingia mitaani kuanzia Bahrain hadi Pakistan kuyapinga.
Al-Nimr alikuwa mtu muhimu katika maandamano ya Washia wachache wa Saudi Arabia, yaliyohamasishwa na uasi wa umma katika mataifa kadhaa ya Kiarabu, hadi alipokamatwa mwaka 2012.
Alitiwa hatiani kwa makosa ya ugaidi, lakini alikanusha kuchochea vurugu. Kiongozi wa juu kabisa nchini Iran, Ayatollah Ali Khomenei, alisema Saudi Arabia italipa gharama kubwa kwa mauaji ya Nimr.
Aituhumu Tehran kwa kuendeleza sera za kibabe.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA