Tuesday 2 February 2016

EPUKA MAKOSA HAYA 7 ILI KUANZA SIKU VIZURI

Kila siku ni nafaasi nyingine ya kuleta maendeleo kwako, familia yako, na kwa taifa kwa ujumla. Waswahili wanasema nyota njema huonekana asubuhi, je unaanza siku vizuri?
Lakini pengine ni vizuri kuuliza, siku nzuri inaanzaje? Kwa mtazamo wangu mie ni kuwa, siku nzuri huanza baada ya kupata usingizi mzuri kwa masaa muafaka – masaa 6 hadi 8. Vingine hufuata baada ya hapa, maana usingizi ni kitu muhimu kuliko chochote kile.
Je kuna vingine zaidi?
Bila shaka. Kuna vingine vingi muhimu vya kuzingatika kwa siku yako. Katika mada yetu ya leo tunaangalia kasumba 7 muhimu za kuepuka ili kuwa na siku njema yenye mafanikio.

1. Kusongeza alarm mbele

Au ningeweza kusema – kutokulala vizuri. Mie sishauri kabisa kulala na alarm, maana kuamka kwa kutega alarm inaonyesha jinsi gani ambayo hupati kulala vizuri usiku. Kawaida mtu anatakiwa kulala masaa 6 hadi 8. Unapotega alarm inaonyesha unalala muda mfupi kupita haya masaa, ambayo ni mbaya kiafya.
Sasa, inapobidi kulala na alarm, hakikisha hausogezi muda mbele. Pale alarm inapolia tu amka na anza siku yako vizuri. Mchezo wa kusogeza mbele dakika 5 au 10 zitakuharibia mood yako mapema, hivyo bora amka na anza siku.

2. Unaoga maji ya moto

Je unapenda kuoga maji ya moto asubuhi ? Hili ni kosa kwa sababu kuu mbili.
  • Kwanza, maji ya moto sana si mazuri kwa afya ya ngozi yako - hufanya ngozi kuzeeka mapema.
  • Pili, utafiti unaonyesha kuwa kuoga maji ya moto kunakufanya ujihisi uchovu na usingizi zaidi. Hivyo unaweza kuhisi kurudi kitandani kuendelea kulala.
Njia mbadala ni kuoga maji ya uvuguvugu. Haya ni maji yanayokupa nguvu kuanza siku. Kama unataka kuoga maji ya moto, basi subiria usiku ili upate kulala vizuri zaidi.

3. Unasahau kunywa maji

Watu wengi wana kasumba ya kunywa kahawa balada ya maji wakishaamka. Pengine ni kasumba kuwa kahawa huwafanya wajisikie vizuri na kuwapa ari ya kufanya kazi zaidi. Lakini si kweli. Maji ndio kitu muhimu zaidi asubuhi maana hukupa nguvu zaidi na kukufanya kuwa na ari ya kufanya kazi zaidi. Badilisha mwenendo, badala ya kahawa, anza na chai. Muhimu zaidi, kama utaweza kunywa maji ya limao, faida zake ni nyingi kama ilivyoelezewa hapa.

4. Unaacha staftahi

Je wewe ni mtu wa kudharau kupata kifungua kinywa kila asubuhi ? Basi jua kuwa hii siyo tabia nzuri. Kifungua kinywa ni muhimu sana mwilini sababu inakata njaa na kuupa mwili nguvu iliyopoteza usiku kucha wakati umelala. Unaweza kuangalia zaidi kwenye makala yetu ya nyuma hapa.

5. Unawaza sana majukumu

Usiwe mtu wa kuwaza majukumu mengi sana yanayokukabili kwenye siku yako mara tu ukishaamka. Badala ya kuwaza majukumu na kazi inayokukabili kwa siku yako, anza kwa shukrani na kufikiria vitu unavyopenda, ni njia nzuri ya kuamka asubuhi ili kuanza siku kwa amani na mtazamo chanya.

6. Unaanza mazoezi mara tu baada ya kuamka

Sikatai, mazoezi ni njia nzuri ya kupata nguvu mwilini, lakini siyo jambo la kwanza kulifanya mara tu baada ya kuamka. Unatakiwa kufahamu kuwa kila kitu kitaenda sawa kama utaanza kwa kujali mwili wako, hivyo pata chakula au kunywa maji ya kutosha. Mazoezi yatafuata baadae.

7. Kutunza mwili wako

Wengi wanapenda kukurupuka na kwenda kazini au shule bila kujali muonekano wao. Hii siyo nzuri. Ili kujiamini na kuwa na Amani, ni vizuri kama utachukua muda kujali mwili na afya yako. Tengeneza nywele, vaa vizuri na tembea kwa kujiamini. Hii ni njia bora ya kukufanya kuanza siku kwa Amani na mtazamo chanya zaidi.
Je wewe unafanya kosa gani katika haya?

-Nakutakia siku Njema

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA