Monday 1 February 2016

GUARDIOLA ASAINI RASMI KUINOA MANCHESTER CITY 2016-2017

KOCHA Pep Guardiola amesaini Mkataba wa miaka mitatu kuifundisha Manchester City baada ya kuthibitishwa Manuel Pellegrini ataondoka Etihad mwishoni mwa msimu.
Pellegrini alifichua habari hizo katika Mkutano na Waandishi wa Habari leo kuelekea mchezo dhidi ya Sunderland kesho, wakati City imesema imekuwa ikimuhitaji Guardiola tangu mwaka 2012.
City imekuwa ikiendesha kwa siri mipango ya kumchukua kocha impendaye, Guardiola kabla ya leo kuweka wazi atajiunga na timu.
Pep Guardiola amesaini Mkataba wa miaka mitatu kujiunga na Manchester City msimu ujao

MATAJI ALIYOSHINDA PEP GUARDIOLA 

BARCELONA:
La Liga: 2008–09, 2009–10, 2010–11
Copa del Rey: 2008–09, 2011–12
Supercopa de España: 2009, 2010, 2011
Ligi ya Mabingwa ya UEFA: 2008–09, 2010–11
Super Cup ya UEFA: 2009, 2011
Klabu Bingwa ya Dunia ya FIFA: 2009, 2011
BAYERN MUNICH: 
Bundesliga: 2013–14, 2014–15
DFB-Pokal: 2013–14
Super Cup ya UEFA: 2013
Klabu Bingwa ya Dunia ya FIFA: 2013
Pellegrini amesema klabu haitaendelea naye baada ya kumakliza msimu na tayari kocha mpya amepatikana.
Taarifa ya Man City imesema; "Manchester City inaweza kuthibitisha kwamba katika wiki za karibuni imekuwa ikishughulikia kukamilisha Mkataba na Pep Guardiola awe kocha Mkuu wa MCFC kwa msimu wa 2016/17 wa Ligi Kuu ya England kuendelea.
"Mkataba ni wa miaka mitatu. Majadiliano hayo ni matokeo mijadala ya mwaka 2012. Kwa heshima yetu kwa Manuel Pellegrini na wachezaji, klabu inataka kuweka wazi uamuzi wake kwa jamii ili kuzuia tetesi zisizo za kawaida. 
Sasa Pellegrini ataendelea na kazi Manchester City hadi mwishoni mwa msimu kabla ya kumpisha kocha mpya, Guardiola ambaye kwa sasa anafundisha Bayern Munich ya Ujerumani iliyomchukua kutoka Barcelona ya Hispania. 

Manuel Pellegrini amethibitisha ataondoka Manchester City mwishoni mwa msimu kumpisha Guardiola

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA