MARTIAL AINUSURU MAN U KOMBE LA FA,SASA KURUDIANA NA WESTHAM
Mshambuliaji Anthony Martial akishangilia baada ya kuifungia Manchester United bao la kusawazisha dakika ya 83 dhidi ya West Ham United katika mchezo wa Robo Fainali Kombe la FA England usiku huu Uwanja wa Old Trafford timu hizo zikitoa sare ya 1-1.
Bao la West Ham limefungwa na Dimitri Payet dakika ya 68 kupitia mpira wa adhabu uliopigwa kwa ustadi wa hali ya juu na sasa timu hizo zitarudiana kuwania kwenda Nusu Fainali ya michuano hiyo.
0 comments:
Post a Comment