Thursday 26 May 2016

ARSENAL YATAMBULISHA 'MIDO' MPYA GRANIT XHAKA KUTOKA BUNDESLIGA

Kiungo mpya wa Arsenal,Granit Xhaka akiwa amepozi na jezi ya timu hiyo baada ya kukamilisha usajili wa Pauni Milioni 35 kutoka Borussia Monchengladbach ya Ujerumani.

UHAMISHO wa Granit Xhaka kutua Arsenal umeiva bada ya picha za mchezaji huyo akipozi kwa ajili ya kupigwa picha kwenye uwanja wa mazoezi ya klabu hiyo wa London Colney kuvuja. Kiungo huyo, 23, aliwasili London Ijumaa iliyopita kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya afya kabla ya kusaini mkataba wa miaka minne na Arsenal na picha za Xhaka akiwa ametinga jezi mpya za Arsenal zitakazovaliwa msimu ujao wa 2016/17, ambazo pia bado hazijatambulishwa rasmi. 

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uswisi amekuwa akifuatiliwa na Arsene Wenger kwa miezi kadhaa na baada ya kuafikiwa kwa ada ya uhamisho ya pauni mil 33.3 na klabu  yake ya Borussia Monchengladbach, anakuwa mchezaji wa kwanza kuwasili Arsenal katika kipindi hiki cha usajili kinachotarajiwa kuwa ‘bize’. Mtumiaji wa ukurasa wa Twitter, Valon Demiri ambaye maskani yake ni Kosovo, aliposti picha hizo kwenye mtandao wa kijamii baada ya kuripotiwa kuzipata kutoka kwa mtu wa karibu na Xhaka.

 Kiungo huyo ametua London na wazazi wake, kaka yake na mkewe kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya afya na kupozi kwa ajili ya picha kabla ya kutangazwa rasmi kwa usajili huo.



0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA