Tuesday 10 May 2016

HAWAJATOSHEKA!!!YANGA YAHALALISHA UBINGWA KWA MBEYA CITY (2-0)


YANGA imezidi kuupendezesha ubingwa wake wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kufuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mbeya City jioni ya leo Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.
Yanga sasa inafikisha pointi 71, baada ya kucheza mechi 28 na ikiwa imebakiza mechi mbili dhidi ya Ndanda FC na Majimaji kukamilisha msimu.
Hadi mapumziko, tayari Yanga walikuwa mbele kwa bao 1-0 lililofungwa na beki Mtogo, Vincent Bossou.
Bossou alifunga bao hilo kwa kichwa dakika ya 15, akimalizia krosi ya beki mwenzake, Juma Abdul kutoka kulia aliyeanzishiwa kona fupi na winga Simon Msuva.

Amissi Tambwe akipongezwa na wenzake baada ya kufunga bao la pili
Beki Mtogo wa Yanga akikimbia kushangilia baada ya kuifungia timu yake bao la kwanza leo


Hata hivyo, Yanga ilipoteza wachezaji wake wawili kipindi cha kwanza, mfungaji wa bao Bossou na kiungo Mkongo Mbuyu Twite ambao wote waliumia.
Nafasi ya Twite ilichukuliwa na Salum Telela dakika ya nane na Kevin Yondan alichukua nafasi ya Bossou dakika ya 29.
Kwa ujumla Yanga ilitawala mchezo kipindi cha kwanza na ingeweza kuondoka inaongoza kwa mabao zaidi kama si kosakosa za wazi mbili tatu.
Kipindi cha pili, nyota ya wana Jangwani iliendelea kung’ara na kuzidi kuwafunika wenyeji Mbeya City uwanjani.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Amissi Tambwe akafunga bao lake la 21 katika Ligi Kuu msimu huu kuipatia Yanga bao la pili dakika ya 84 kwa shuti la nje kla 18.
Mshambuliaji wa Zimbabwe, Donald Ngoma hakuwa mwenye bahati leo kutokana na kukosa mabao mawili ya wazi, moja kila kipindi wakati Simon Msuva alipoteza nafasi moja nzuri kipindi cha pili. 

KWA HISANI YA BIN ZUBERY BLOG

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA